Sunday, February 1, 2015

AMKA NA MAGAZETI NA KUMEKUCHABLOG

MAGAZETI YA LEO YANALETWA KWENU KWA HISANI YA NEW AGE EDUCATION CENTRE, KITUO CHA ELIMU TANGA, WAPO MKABALA NA SHIRIKA LA UMEME TANZANIA TANESCO, MOB, 0717 713866
















 Hutopitwa na habari yoyote na tangakumekucha itakupa kila habari inayotufikia na tembelea kila wakati kupitia blog hii

IVORY COAST YATINGA NUSU FAINAL

Ivory Coast yaingia Nusu fainali ya Afcon .

Ivory-coast

Timu ya taifa ya Ivory Coast imekuwa timu ya nne kufuzu hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la mataifa ya Afrika baada ya kushinda mchezo wao dhidi ya timu ya taifa ya Algeria .
Ivory Coast imeifunga Algeria kwa matokeo ya 3-1 katika mchezo ambao ulimalizika ndani ya dakika 90 .
Mabao ya Ivory yalifungwa na Wilfred Bony ambaye alifunga mabao mawili huku Gervinho akifunga bao moja .
Bao pekee la Algeria lilifungwa na Hilal Soudani kwenye kipindi cha pili .
Kwa matokeo haya Ivory Coast watacheza nusu fainali na Congo Drc huku Ghana wakicheza nusu fainali na wenyeji wa michuano hii Equatorial Guinea.

GHANA YAFUZU FAINAL AFCON

Ghana yafuzu nusu fainali Afcon .

Football - 2011ACQ - Ghana v Swaziland - Accra Sports Stadium

Michuano ya kombe la mataifa ya Afrika imeendelea jana kwa kushuhudia mchezo mmoja wa hatua ya robo fainali ukizikutanisha Ghana pamoja na Guinea .
Katika Mchezo huo Ghana walifanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali wakiwafunga Guinea kwa mabao matatu bila .
Ghana walianza kazi mapema wakifunga bao  kwenye dakika ya nne kupitia kwa winga Christian Atsu .
Black Stars walipata bao la pili kwenye kipindi cha kwanza mfungaji akiwa Kwessi Appiah bao ambalo liliua matumaini ya Guinea .
Mwanzoni mwa kipindi cha pili Ghana walifunga bao la tatu mfungaji akiwa Christian Atsu tena na kuikatia timu yake tiketi ya kufuzu hatua ya nusu fainali .
Nafasi ya mwisho kwenye hatua ya nusu fainali itafahamika saa chache zijazo wakati mchezo wa mwisho wa roo fainali utakaowakutanisha Ivory Coast na Algeria utakapopigwa .
Hadi sasa timu tatu tayari zimefuzu hatua ya nusu fainali nazo ni wenyeji Equatoarial Guinea , Ghana pamoja na Jamhuri ya kidemokrasi ya kongo .

HEBU CHEKI TENA PICHA ZA MTANANGE WA PELE EMARETEES

Arsenal wafanya mauaji 

ARSENAL

Washika bunduki toka jijini London Arsenal hii leo (jumapili) wamefanikiwa kuwafunga Aston Villa kwa ushindi mnono wa 5-0 katika mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Emirates katika muendelezo wa ligi kuu ya England .
Arsenal walianza mchezo huo kwa kasi wakifunga bao la haraka kwenye dakika ya 8 mfungaji akiwa mshambuliaji raia wa Ufaransa Olivier Giroud baada ya pasi ya beki Per Mertersecker .
Arsenal walifunga bao la pili kupitia kwa kiungo mshambuliaji Mesut Ozil ambaye alipokea pasi ya Giroud na kuukokota mpira kabla ya kupiga shuti dogo lililompita kipa wa Aston Villa Brad Guzan .
Mshambuliaji Olivier Giroud akiifungia Arsenal bao la kwanza kwenye mchezo wa leo .
Mshambuliaji Olivier Giroud akiifungia Arsenal bao la kwanza kwenye mchezo wa leo .
Theo Walcott aliifungia Arsenal bao la tatu kwenye dakika ya 63 baada ya kupewa pasi na Santi Cazorla ambaye alikuwa moja kati ya wachezaji waliong’ara katika mchezo wa leo .
Bao la nne lilifungwa kwa njia ya penati baada ya kipa wa Aston Villa Brad Guxzan kumchezea vibaya mshambuliaji chipukizi Chupa Akpom , Santi Cazorla alipiga penati hiyo na kuipa timu yake bao linguine huku Aston Villa wakiendelea kupata wakati mgumu .
Theo Walcott alifunga bao la pili kwenye mchezo dhidi ya Aston Villa.
Theo Walcott alifunga bao la tatu kwenye mchezo dhidi ya Aston Villa.
Wakati mchezo ukielekea mwishoni , beki wa kushoto Hector Bellerin alifunga karamu ya mabao baada ya kuipa Arsenal bao la tano .
Ushindi huu unawafanya Arsenal kuchupa hadi nafasi ya tano wakiwa na pointi 42 , pointi moja nyuma ya Man United walioko kwenye nafasi ya nne .
Kiungo  Mesut Ozil naye alikuwa moja ya wafungaji .
Kiungo Mesut Ozil naye alikuwa moja ya wafungaji .

ARSENAL YAFANYA MAUWAJI ENGLAND

Arsenal Vs Aston Villa – nimekusogezea matokeo hapa

(null)
Wakiwa hawajafunga goli hata moja tangu December 20 – wakati Christian Benteke alipofunga goli dhidi ya Manchester United, Aston Villa leo walisafiri hadi jijini London kwenda kukipiga na Arsenal.
Mchezo huo uliomalizika hivi punde umeisha kwa Villa kucheza takribani dakika 600 bila kufunga goli hata moja – baada ya kukubali kupewa kipigo kizito zaidi msimu huu cha magoli 5-0.
Olivier Giroud alianza kuifungia Arsenal baada ya pasi nzuri ya Ozil, kabla ya mjerumani huyo nae kuongeza la pili na Theo Walcott akafunga la tatu na kuipeleka Gunners mapumziko wakiwa mbele kwa 3-0.
Kipindi cha pili Santi Cazorla akafunga la nne kwa mkwaju wa penati kabla ya Hector Bellin kufunga la tano mwishoni kabisa mwa mchezo huo.

HEBU CHEKI MTANANGE ULIVYOKUWA PALE UWANJA WA TAIFA

Yanga Sc Vs Ndanda FC imemalizika. Matokeo na Pichaz nimekusogezea hapa…

.
.
Ligi Kuu Tanzania Bara imeendelea leo February 1, 2015 katika Uwanja wa Taifa Dar, ambapo timu ya Young Africans (Yanga) walikuwa wakipambana na Ndanda FC.
Mpaka dakika tisini zinakamilika matokeo Yanga SC na Ndanda FC wametoka bila kufungani  (0-0).
.
.
.
.
Matokeo ya michezo ya leo yanawafanya Yanga washindwe kuwafikia Azam Fc kwenye kilele cha msimamo wa ligi ya Tanzania Bara ambapo hadi sasa wana pointi 19 wakiwa wamezidiwa kwa pointi mbili na Azam wenye pointi 21 .
.
.
DSC08983
.
DSC08985
.
Picha zote ni kutoka kwenye screen ya Azam TV.
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

YANGA YASHIKWA UWANJA WA TAIFA

Yanga yabanwa kwenye ligi kuu Tanzania Bara.

yanga

Ligi kuu ya soka Tanzania Bara imeendelea hii leo kwa michezo miwili iliyopigwa jijini Dar-es-salaam pamoja na huko mkoani pwani ambako timu nne zilikuwa viwanjani zikisaka pointi tatu muhimu .
Jijini Dar-es-salaam uwnaja wa taifa ulishuhudia mchezo kati ya mabingwa wa zamani wa ligi hiyo Dar-es-slaam Young Africans dhidi ya timu iliyopanda daraja msimu huu ya Ndanda Fc toka Mtwara .
Mpaka kipenga cha mwisho kinapulizwa kuashiria mchezo huo kumalizika hakukuwa na timu iliyoweza kumtambia mwenzie baada ya timu hizo mbili kutoka sare ya bila kufungana .
Hata hivyo Yanga watajilaumu wenyewe kwa kushindwa kuondoka na ushindi baada ya kutengeneza nafasi kadhaa za wazi ambazo kama washambuliaji wake wangekuwa makini basi Yanga ingeweza kushinda .
Mshambuliaji raia wa Liberia Kper Sherman alikosa bao la wazi .
Mshambuliaji raia wa Liberia Kper Sherman alikosa bao la wazi .
Katika mchezo mwingine uliopigwa huko mkoani Pwani kwenye uwanja wa Mabatini wenyeji Ruvu Shooting waliwafunga Stand United kwa mabao mawili kwa moja .
Ruvu   Shooting walifunga mabao yao kupitia kwa Juma Mpakala kwenye dakika ya tano ya mchezo huku bao la ushindi likija kupitia kwa Yahya Tumbo kwneye dakika ya 89 na Stand United wakafunga kupitia kwa Hamis Thabit .
Matokeo ya michezo ya leo yanawafanya Yanga washindwe kuwafikia Azam Fc kwenye kilele cha msimamo wa ligi ya Tanzania Bara ambapo hadi sasa wana pointi 19 wakiwa wamezidiwa kwa pointi mbili na Azam wenye pointi 21 .

SHILOLE ALONGA KUHUSU KUMPIGA KIBAO NUH

Ya Shilole kuhusu kumpiga kibao Nuh Mziwanda, na Nuh anazungumza pia hapa.

Screen Shot 2015-02-01 at 3.43.28 PMDecember 2014 Mwimbaji Shilole alivishwa pete ya uchumba na Nuh Mziwanda ambaye pia ni msanii, siku hii ilikua siku ya birthday ya Shilole.
Baada ya hapo waliendelea kuchukua headlines ila iliyokua nzito zaidi ni Shilole kudaiwa kumpiga kibao Nuh Mziwanda mbele za watu wakati wa consert  iliyofanyika viwanja vya Leaders Club Dar es salaam.
Baada ya hapo Shilole aliomba msamaha kupitia page yake ya instagram kwa mashabiki na kwa mpenzi wake akisema ‘Binafsi sikupenda ila ni hasira tu lakini haitotokea tena‘ alafu post inayofata Shishi akaandika ‘Naamini Nuh ni mwanaume sahihi kwangu maana hawezagi kurusha hata ngumi japo namchokozaga mie mjeuri tu
Hutopitwa na lolote na niko tayari mtu wangu kukupatia kila kinachonifikia muda wowote, kupitia www.tangakumecha.blogspot.com

MANCHESTER YAHAHA KUMBAKIZA DAVID DE GEA

Manchester United hali mbaya kwa David De Gea.

David-De-Gea-of-Manchester-United-gestures

Tetesi kuhusu mustakabali wa kipa Mhisapnia David De Gea ndani ya klabu ya Manchester United zimezidi kuibuka ambapo kila siku ameendelea kuhusishwa na kujiunga na mabingwa wa ulaya Real Madrid ambao wametajwa kuwa na mpango wa kumsajili kipa huyo .
Taarifa toka England na Hispania zinasema kuwa wawakilishi wa kipa huyo wanataka kuwepo na kipengele kinachoruhusu kipa huyo kuuzwa ndani ya mkataba mpya ambao anatarajiwa kuusaini .
De Gea amebakiza miezi 18 kabla ya kumaliza mkataba wake wa sasa na United na klabu hiyo imekuwa katika mkakakati wa kuhakikisha kipa huyo anasaini mkataba mpya ambao una maslahi yaliyoboreshwa tofauti na mkataba wake wa sasa .
United imemsajili kipa wa zamani wa Barcelona Victor Valdez ambaye huenda akawa mrithi wa David De Gea endapo atakimbilia Real Madrid.
United imemsajili kipa wa zamani wa Barcelona Victor Valdez ambaye huenda akawa mrithi wa David De Gea endapo atakimbilia Real Madrid.
Katika kuhakikisha kipa huyo anabaki United , timu hiyo imejiandaa kumfanya De Gea kuwa kipa anayelipwa fedha nyingi kuliko wote duniani kwa mshahara wa paundi laki mbili kwa wiki lakini wawakilishi wa kipa huyo wamekuwa kikwazo kwa harakati hizi za United .
De Gea kwa mbali amekuwa mchezaji bora kwa timu yake ambapo kwenye michezo kadhaa amekuwa akiikoa huku akionyesha kiwango cha juu hali ambayo imemfanya atajwe kuwa moja ya makipa bora duniani .
Real Madrid kwa muda mrefu wamekuwa na shauku ya kumsajili Mhispania huyu ambaye kwa upande mwingine ameonyesha dhamira ya kurudi nyumbani kwao jijini Madrid .
Kitendo cha United kumsajili kipa wa zamani wa Barcelona Victor Valdez kimeongeza fununu za kuondoka kwa De Gea na mpaka sasa bado uongozi wa United unahaha kuhakikisha unambakiza kipa huyo .

BAADA YA KUFA MAMA YAKE KWA MADAWA YA KULEVYA, MTOTO NAE ARITHI UBWIAJI

Baada ya Whitney Houston kufariki kwa dawa za kulevya, vipi kuhusu hili la mwanaye?

bobiMtoto wa marehemu Whitney Houston, aitwaye Bobbi Kristina Brown amekutwa katika hali mbaya nyumbani kwao katika mji wa Georgia jana na kukimbizwa hospitali.
Inasemekana mtoto huyo amekua akitumia madawa ya kulevya ambayo ndiyo yaliyosababisha kifo cha mama yake
Mume wake Nick Gordon alikutwa akiwa na binti huyo na sasa anahojiwa na polisi kuhusiana na Bobbi Kristina.
with mom
Bobbi Kristina Brown akiwa na marehemu mama yake Whitney Houston
Hata hivyo hakukua na maelezo yoyote kutoka kwa daktari baada ya kutokuwepo na msemaji katika hospitali ya North Fulton alikopelekwa.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

AMUUWA MKE WAKE KISA AMEMZALIA MTOTO WA KIKE

Amuua mke wake baada ya kujifungua, kisa ni jinsia ya mtoto aliyezaliwa

waya
Wanandoa wengi linapokuja suala la kupata watoto wengi wao hupanga na kuwa na matarajio mengi juu ya ujio wa watoto wanaowatarajia, lakini pia kunakuwepo na chagua la jinsia ya mtoto atakayezaliwa ambalo huamuliwa na pande zote mbili.
Lakini pia Matukio ya unyanyasaji yameendelea kuwepo baina yao hasa pale mwanaume anapotaka kitu fulani na kisifanikiwe kwa wakati huo kama ambavyo mwanaume huyu Vuysi Turan raia wa Uturuki kuamua kumuua mkewe siku moja baada ya kujifungua mtoto wa pili wa kike kitendo kilichomkasirisha baada ya kutaka mtoto wa kiume.
Turan amehukumiwa adhabu ya kifo baada ya kumpiga mkewe na shoti ya umeme kisa tu amemzalia mtoto wa kike wakati yeye alikua akitaka wa kiume.
Kwa mujibu wa mahakama iliyomuhukumu mwanaume huyo adhabu ya kifo ilieleza kuwa, mwanamke huyo baada ya kutoka hospitali kujifungua mumewe alinunua nyanya za umeme na kuziwasha kisha kumchoma nazo miguuni hadi kufariki dunia.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

YALIYONIKUTA TANGA (9)



HADITHI

YALIYONIKUTA TANGA (9)

ILIPOISHIA TOLEO LILILOPITA

“Leo nimekwisha!” nikajiambia. Nilikuwa sina pa kukimbilia. Lakini nilikwishatambua kila kitu.

Sikujua niliwezaje kuwasiliana na yule msichana hadi nikafika katika nyumba ile ya mauti! Kusema kweli nilijipeleka mwenyewe!

Kwa vyovyote vile, nilijiambia, nyumba ile haikuwa ya binaadamu wa kawaida. Yule bibi alikuwa jini! Na kama alikuwa jini, niliendelea kujiambia, sitaweza kunusurika mle ndani.

Licha ya kutoka pale uani, yule bibi hakushituka. Aliendelea kuchimba lile shimo kwa bidii.

Hakuna binaadamu yeyote anayekubali kufa kirahisi, nikageuka haraka na kurudi nilikotoka. Wakati nafika kwenye mlango wa  mbele, mlango huo ulikuwa unafunguliwa. Nilijificha nyuma ya mlango. Akaingia yule msichana.

Na yeye alikuwa uchi na alikuwa na umbile sawa na lile la mama yake. Alikuwa amejaa manyoya mwili mzima na miguu yake ilikuwa ya kwato nyeusi. Mkononi alikuwa ameshika upanga.

Mwenzake alikuwa mwanaume. Na yeye alikuwa kama walivyokuwa wenzake. Hapo nikagundua kuwa yule mama na binti yake waliokuwa wakiuza vitu vya dhahabu, walikuwa ni majini lakini watu hawakuwa wakijua.
  
SASA ENDELEA

Ule upanga aliokuwa ameushika Maimuna ulikuwa wa nini? Nikajiuliza.

Lakini jibu lilikuwa wazi kuwa upanga huo ulikuwa ni kwa ajili ya kuchinja kichwa changu. Bila shaka ndio uliotumika kumchinja Sajenti Erick.

Usiku huo ulikuwa wa balaa kwangu. Nilijuta kulaimisha mawasiliano na yule msichana hadi yakanikuta yaliyonikuta. Lakini nilihisi kukutana tena na majini hao ilikuwa ni mipango yao ya kutukomoa kama walivyomkomoa Sajenti Erick kutokana na ile dhambi tuliyowafanyia.

Kosa langu ni kuwa nilijiingiza kichwa kichwa mara tu Maimuna aliponitumia meseji aliyodai kuwa haikuwa yangu bali alikosea namba. Ilikuwa tamaa yangu ya wasichana iliyopelekea nifike mahali hapo pa mauti.

Maimuna na mwenzake walipoingia hawakuufunga ule mlango wa nje. Kama wangeufunga wangeniona.

“Yuko wapi?” Maimuna akauliza alipoona sikuwepo mahali ambapo nilikuwa nimelala. Akakimbilia uani. Mwenzake aliyekuwa naye akamfuata.

Hapo ndipo nilipopata upenyo wa kutoka. Nilipotoka nje nilianza kukimbia. Jambo lililonishangaza ni kuwa nilijiona niko kwenye msitu wa kutisha. Nilikuwa najikimbilia ovyo bila kujua nilikuwa ninakwenda wapi.

Nikatoa simu yangu mfukoni na kuwapigia polisi wenzangu ili nipate msaada. Wakati napiga simu nilikuwa nakimbia. Simu ilipokelewa. Aliyepokea alikuwa mwanamke. Nikamwambia.

“Mimi ni Martin Lazaro wa CID nimepatwa na matatizo, naomba msaada wenu”

“Mimi ni Maimuna. Uko wapi Martin, nakutafuta?” Sauti ikaniuliza kutoka simu ya upande wa pili. Mara moja niliitambua sauti ya Maimuna.

Nikaikata simu haraka kwa kuona nilikuwa nimekosea namba na kumpigia yule msichana muuaji niliyekuwa namkimbia.

Nikasimama na kuiangalia kwa makini namba ya polisi kisha nikaipiga. Nilikuwa nimesimama. Moyo ulikuwa ukinienda mbio na nilikuwa nahema kama niliyekuwa nafukuzwa.

Simu ikapokelewa tena. Kabla ya kusema chochote nikaisikia tena sauti ya Maimuna ikiniuliza.

“Uko wapi?”

Moyo ukanilipuka kwa hofu. Nikaitazama ile namba. Nikaona ni namba ya polisi lakini aliyepokea alikuwa Maimuna. Nikaamini kuwa wale walikuwa majini kweli.

Nikakata simu na kuendelea kukimbia. Simu ikawa inapigwa. Nikasimama na kutazama namba iliyokuwa inapiga, nikaona namba ya polisi.

Nikaipokea haraka.

“Jamani nina matatizo, nikipiga simu inakwenda kwingine…”

“Inakwenda wapi?” Sauti iliyoniuliza ilikuwa ya Maimuna.

“Wewe nani?” nikamuuliza kwa kutaharuki.

“Mimi Maimuna umenisahau mara moja hii, wakati tulikuwa wote hapa nyumbani…”

Nikakata ile simu na kuendelea kukimbia. Kutahamaki nikajiona nimetokea mbele ya ile nyumba ya Maimuna.

Nilikuwa nakimbia lakini nilipiga breki ya ghafla, nikaitazama ile nyumba iliyokuwa mbele yangu. Nilihakikisha kuwa ilikuwa ndio ile ile nyumba ya Maimuna na mahali palikuwa pale pale. Kwa maneno mengine ni kwamba nilikuwa nimerudi hapo hapo.

Mlango ulikuwa umefungwa, nikaona unafunguliwa. Sikujua nani angetoka, nikageuka na kuanza tena kukimbia. Sasa nilikuwa kama mwendawazimu niliyekuwa nikijikimbilia ovyo.

Wakati ninakuja katika eneo lile hakukuwa na msitu. Kulikuwa na vichaka tu na miti michache ya mikoroshi. Sasa niliona ajabu kuona msitu wa kutisha. Sikuweza kujua jinsi msitu huo ulivyotokea.

Simu yangu ilkuwa inaita lakini sikushughulika nayo tena, niliendelea kukimbia tu. Nia yangu ilkuwa kutokea katika barabara au njia ya watembea kwa miguu lakini sikuona njia wala barabara.

Ghafla niliona nyumba kwa mbali. Ilikuwa inawaka taa kwa nje, nikakimbilia kwenye nyumba hiyo ili kuomba msaada. Nilipofika niligonga mlango.

“Jamani naomba msaada…jamani naomba msaada” nikasema huku nikiendelea kugonga.

Baada ya muda kidogo mlango ukafunguliwa.

“Karibu” Bibi mmoja aliyekuwa amejitanda shuka nyeupe akanikaribisha.

Nikamueleza ule mkasa ulionifika. Nilipomaliza kumueleza akapandisha juu gauni lake na kuniuliza.

“Hao watu unaosema wana kwato, kwato zao ni kama hizi?” alinionesha miguu yake.

Nilipoitazama nikaiona ina kwato kama zile za kina Maimuna! Nikashituka na kumtazama yule bibi usoni. Sasa  nikamuona vizuri. Alikuwa ndiye yule aliyekuwa akichimba kaburi kule uani kwa Maimuna.

“Eh! Amefikaje huku!” nikajiuliza kabla ya kugeuka nyuma na kuanza tena kukimbia.

“Mbona unakimbia?” akaniuliza.

Sikumjibu, niliendelea kukimbia.

“We kijana hebu njoo…” Yule bibi alinipigia kelele.

Nikageka na kumtazama. Alikuwa ametoka nje akiniangalia. Nikajipoteza kwenye msitu. Nilikuwa nimechoka na moyo ulikuwa ukinienda mbio sana. Nilijua kuwa wakati wowote ningeweza kuanguka na kuzimia.

Kitisho nilichokipata kilikuwa kikubwa na kiliutikisa moyo wangu hasa. Sikuwa mtu wa kuamini mashetani lakini siku ile niliamini kuwa mashetani wapo na wanatisha. Licha ya kujitahidi kukimbia muda wote nilijua kuwa nitakufa kwani sikuwa na ujanja wa kutoka kwenye msitu huo. Ile hofu peke yake ingweza kuniua.

Hapo nikaanza kumlaumu Sajenti Erick kwani yeye ndiye aliuleta mpango ule wa kwenda kumkamata yule bibi na kumbambikia kesi ya madawa ya kulevya.

Je nini kitatokea? Tukutane hapo kesho
Usiache kutembelea blog hii kila wakati kwa mambo mazuri na matamu kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

DUNIA NA MAAJABU YAKE, HEBU ANGALIA PICTURES NI WATU AU MAJINI

SHUHUDIA TATTOO ZA AJABU

Mary Jose Cristerna, raa wa Mexico akionyesha tottoo zake alizojichora ambapo inadaiwa kuwa wataalamu wa kuchora nchini humo wamekuwa wakijipatia mamilioni ya fedha baada ya watu wengi kupendezwa na tottoo hizo.
Ms Cristerna, akionyesha tottoo zake alizojichora kwenye ulimi na chni ya mdomo wake ambapo amedai kuwa staili hiyo imekuwa gumzo akipita mitaa ya jiji la Mexico na watu wengi kuipenda.
As well as extreme modification to her face, she offers people the key to hear heart, pictured

Huyu ni raia wa Venezuelan akiwa amejichora tottoo ya mtindo wa red 


Kala Kaiwi, pictured, holds the world record for the non-surgically made stretch earlobes, at 109mm wide
Kala Kaiwi, pictured, describes himself as a body modification artist from Hawaii

Colombian Carlos Dehaquiz, who looks lizard-like, is one of the more normal exhibitors at the event

This woman hitches up her jeans to show of the design on her left leg, pictured which includes a skull
Hutopitwa na jambo lolote mtu wangu na niko tayari kukupatia kila kinachonifia wakati wowote  kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

AMKA NA MAGAZETI NA KUMEKUCHA BLOG

Mkusanyiko wa Stori 8 kubwa zilizopewa headlines kwenye Magazeti ya leo February 1, 2015 ziko hapa

cup
NIPASHE
Serikali imeruhusu wanafunzi wa shule za msingi na sekondari waliopata ujauzito kuendelea na masomo wanapojifungua.
Mratibu wa Masuala ya Jinsia wa  Wizara ya Elimu na Mafunzo ya  Ufundi, Chimpaye Marango, wakati wa mjadala wa sababu za kuongezeka kwa idadi ya watoto ya  mabinti wanaokosa elimu baada ya kupata mimba.
Mjadala huo ulioitishwa na  asasi ya kiraia ya uchambuzi wa sera ya Policy Forum iliwakutanisha wadau mbalimbali wa elimu.
Marango alisema lazima wasichana waliopewa ujauzito kuhakikisha wanarudishwa haraka shuleni mara watakapojifungua, vinginevyo hatua kali watachukuliwa watakaowazuia.
Wizara imeliona hilo na tayari imewekwa sera mpya, kwani kumuadhibu kwa kumfukuza shuleni hakutaweza kuwasaidia watoto wa kike kumudu maisha  badala yake tunaongeza umasikini ndani ya jamii:- Marango.
Awali, Dk.  Rebecca Balira, kutoka Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Tiba Afrika (Amref) alisema tatizo la mimba kwa wanafunzi wa kike  limekuwa sugu nchini.
Alisema katika utafiti uliofanyika katika Wilaya za Kilindi, Mkalama, Iringa vijijini na Same jumla ya wanafunzi wa kike 55,000  walishindwa kuendelea na masomo kwa kipindi cha mwaka 2003 hadi 2011.
NIPASHE
Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, ametangaza kuwashughulikia watu wote waliohusika kulihujumu Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), ambalo ‘limekufa’, huku akionyesha masikitiko yake kuona mpaka sasa hatua kali hazijachukuliwa dhidi yao.
Sitta alisema hayo, wakati akijibu hoja za wabunge, waliochangia mjadala kuhusu taarifa za kazi za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na ya Nishati na Madini, kuanzia Januari 2014 hadi Januari 2015, zilizowasilishwa bungeni jana.
Alisema makosa yaliyotendeka huko nyuma dhidi ya ATCL, ni ya ovyo ovyo kabisa na kushauri Bunge liweke utaratibu wa kutunga sheria za kuwabana watu wanaoyatenda.
Sitta alisema hali mbaya iliyopo ATCL inayotokana na deni linaloikabili, inachangiwa kwa kiasi kikubwa na uzembe unaokaribiana na hujuma.
Sina hakika kama wahusika wamepatiwa dawa yao. Si ajabu wanatamba tu, wako mahali fulani tu wanaangalia. Basi kuna udhaifu fulani lazima tuurekebishe ili tuweze kwenda vizuri:-Sitta.
Kuhusu usafiri wa treni ya Dar es Salaam, maarufu kama “Treni ya Mwakyembe“, alisema baada ya mkutano kati ya wizara na Wajerumani unaotarajia kufanyika jijini humo, Jumanne ijayo, itaboreshwa zaidi ya ilivyo hivi sasa.
NIPASHE
Mkazi wa Tabata Mawenzi, Remi Joseph (36) anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuua mkewe kwa kumkata kichwa kwenye nyumba ya wageni ya Friends Corner ya jijini Dar es Salaam.
Aliyeuawa ni Josephena Moshi (35), ambaye alikatwa kichwa na kuchomwa na kitu chenye ncha kali kifuani wakiwa kwenye nyumba ya wageni ya Friends Corner.
Akihojiwa kuhusiana na tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa  Kinondoni, Augustine Senga, alikiri kutokea mauaji hayo.
Senga alisema mwanamke huyo alifariki papo hapo baada ya kushambuliwa na kwamba chanzo cha mauaji hayo hakijafahamika na uchunguzi unaendelea.
Kamanda alipoulizwa kuhusiana na mtuhumiwa huyo kutaka kujiua, alisema kuwa uchunguzi unaendelea.
Bado ni mapema sana kueleza kila kitu hayo niliyokueleza ni taarifa za awali kwani na huyu mtuhumiwa amekutwa na majeraha shingoni, hivyo masuala ya kazi yake na sababu vinachunguzwa:- Senga.
MWANANCHI
Wakati Serikali ikitafuta njia ya kumaliza tatizo la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi ‘albino’ katika Mikoa ya kanda ya ziwa,imedaiwa watoto ambao hawajafikisha umri na kufariki dunia wakati wa kuzaliwa viungo vyao huuzwa kwa waganga wa kienyeji.
Hayo yalibainika juzi mbele ya Katibu tawala wa Mkoa wa Simiyu, Mwamvua Jilumbi katika kikao cha pamoja kilichofanyika katika ukumbi wa KKKT ulioko Bariadi wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa kukomesha vifo vya wajawazito.
Wadau hao walibainisha kuwa hali hiyo hujitokeza kila mara katika hospitali ya Wilaya ya Bariadi na walieza pia mtandao wa wahusika wa viungo hivyo hufanyika kati ya wauguzi na madaktari ambao ndio huzalisha wamama wajawazito.
Wadau hao waliendelea kueleza kuwa viungo hivyo vimekuwa vikiuzwa kuanzia 400,000 hadi 500,000.
MWANANCHI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Aboud Mohamed amesema wananchi hawana imani tena na Jeshi la Polisi kwa kuwa vitendo vya uhalifu vinafanyika, lakini hakuna wanaotiwa mbaroni.
Waziri Aboud alitoa kauli hiyo wakati wa kufunga mkutano wa wakuu waandamizi wa Jeshi la Polisi uliokuwa ukifanyika mjini hapa, huku chombo hicho cha dola kikizidi kurushiwa lawama kutokana na ongezeko la uhalifu ambao umefikia hatua ya vituo vya polisi kuvamiwa na askari kuuawa na kuporwa silaha.
Jeshi hilo pia linalaumiwa kutokana na jinsi linavyoshindwa kushughulikia vurugu kwa weledi na hivyo kujikuta ikitumia nguvu nyingi zinazosababisha wananchi kuuawa na kujeruhiwa.
Waziri Aboud alibainisha kuwa wananchi wengi kwa sasa hawana imani tena na polisi kwa kuwa vitendo vya uhalifu vinafanyika lakini hakuna watuhumiwa wanaokamatwa na kutiwa mbaroni.
Tabu inakuja pale uhalifu unapotokea na polisi kushindwa kuwapata wahalifu… wananchi wanapenda wahalifu wote watiwe mbaroni na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria:- Aboud.
MWANANCHI
Mbunge wa Bukoba Mjini kwa tiketi ya CCM, Khamis Kagasheki amemtuhumu Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuwa ndiye aliyekuza mgogoro wa Bukoba uliosababisha madiwani wa halmashauri kushindwa kufanya vikao, akidai kuwa mtendaji huyo mkuu wa Serikali ameshindwa kuchukua hatua.
Tuhuma hizo za Kagasheki ni za nadra kwa mbunge huyo wa chama hicho tawala kuelekeza kwa mtendaji mkuu wa Serikali na mmoja wa wajumbe wa vikao vya juu vya CCM.
Kagasheki, ambaye alikuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, alitoa tuhumu hizo wakati wa mahojiano maalumu na gazeti hili wiki iliyopita, akisisitiza kuwa ni makosa kuutazama mgogoro huo kuwa ni kati ya yake na meya na akataka ijulikane kuwa kinachoendelea Bukoba ni suala la wizi.
Mgogoro huo wa kisiasa, ambao umedumu kwa takriban miaka miwili na unaotishia kugawanyika kwa CCM, umekolezwa na kufunguliwa kwa kesi tatu ambazo zimezuia utekelezaji wa shughuli za maendeleo na umekuwa ukihusishwa na vita vya ubunge baina ya Kagasheki na Meya wa Manispaa ya Bukoba, Anatory Amani.
Hii ni mara yangu ya kwanza kupata nafasi ya kuzungumzia suala hili. Hakuna unafiki hapa, hili nitalisimamia mahali popote na nitalisema mahali popote kuwa Pinda, ndiye tatizo katika mgogoro huu ulioinyima Bukoba maendeleo:-Kagasheki.
MTANZANIA
Wanakiji  wa Namonge mkoani Geita, wameua watu wawili ambao ni askari wa wanyama pori na  msaidizi wake, baada ya kuwashambulia kwa  mawe, mapanga, rungu na nondo wakiwatuhumu kuwa ni majambazi.
Kufuatia mauaji hayo yaliyotokea wilayani Bukombe,  watu 24 akiwamo ofisa mtendaji wa kijiji hicho wanashikiliwa na polisi.
Tukio hilo limetokea juzi jioni baada ya wananchi hao kukusanyana na kuivunja ofisi ya serikali ya kijiji hicho ambako walinzi hao walikuwa wamehifadhiwa na ofisa mtendaji wa kijiji hicho, Andrea Malise.
Wananchi walioshuhudia mauaji walisema juzi  alasiri watu  watano, mmoja wao akiwa na silaha aina ya SMG walipita kijijini  baadaye  kuingia baa wakiwa na pikipiki lakini safari hiyo bila silaha.
Kutokana na kuonekana wageni wanakijiji walianza kuhoji na kuwasiliana juu ya wageni hao.
Pasipo subira inadaiwa wananchi walianza kuwatupia mawe na kuwashambulia ndipo ofisa mtendaji alipoingilia kati na kuwaweka katika ofisi yake  kukwepa vipigo kutoka kwa wananchi hao.
Hofu ya wananchi inadaiwa inachangiwa na kuwapo kwa matukio  ya kihalifu ya  mara kwa mara katika ukanda huo, likiwamo la mnada wa ng’ombe kuvamiwa na watu wenye silaha Januari 16 mwaka huu na wengine wenye silaha kuingia katika kijiji cha Ilyamchele siku tatu baadaye  na kuwateka wanakijiji baada ya kuwakirimu.
HABARILEO
WAKATI Jeshi la Polisi likilaumiwa kutokana na namna lilivyoshughulikia maandamano ya Chama cha Wananchi (CUF) wiki iliyopita, Serikali imetahadharishwa kuwa makini na harakati za kisiasa zinazotumia mbinu za kuchokoza Jeshi la Polisi na kuvunja sheria halali.
Wakizungumza na gazeti hili wiki hii kuhusu dhana ya udhaifu wa jeshi hilo, baadhi ya watu wakiwemo wasomi wameitaka Serikali kuwa makini na kauli za wanasiasa, ambao wamewahi kushiriki au kutoa matamko ya kihalifu na leo wanatuhumu jeshi hilo.
Baadhi ya matukio ya kihalifu yaliyotajwa kufanywa katika mazingira ya siasa, tamko la maandamano na migomo isiyokoma, bila kibali cha Polisi, lililotolewa hivi karibuni na Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, Freeman Mbowe na udhalilishwaji wa Mkuu wa Wilaya, wakati wa uchaguzi mdogo wa Igunga uliokuwa na ushindani wa kisiasa mwanzoni mwa 2011.
Tahadhari hiyo imetolewa, wakati Serikali ikielezea kuridhishwa na kazi ya kutunza amani nchini inayofanywa na jeshi hilo, na kuagiza lijiandae na siasa za 2015; siasa za kabla ya Kura ya Maoni ya kupata Katiba Mpya na za kabla ya Uchaguzi Mkuu ujao.
Maandamano ya CUF Akitoa tamko kuhusu kudhibitiwa kwa maandamano ya CUF wiki iliyopita, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, akizungumzia hoja ya mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James Mbatia (NCCRMageuzi), kuhusu polisi walivyodhibiti maandamano ya CUF, alisema Prof. Ibrahimu Lipumba, ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, alikaidi zuio la Jeshi la Polisi.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

SERENA WILLIAMS HAKAMATIKI

Serena Williams aendelea kuwakimbiza kwenye Tennis

Serena Wills
Umri wake ni miaka 33, Serena na Venus ni ndugu, mtu na dada yake na wote ni wachezaji wa mchezo wa Tennis, tumeshuhudia mara nyingi namna ambavyo wanafanya vizuri kwenye mchuano hiyo kwa kipindi kirefu duniani na kuvunja rekodi mbalimbali.
Sio mara moja wawili hao wamekutana uwanjani na kushindana, lakini jana January 31 ilikuwa ni fainali ya michuano ya Australia Opens, uwanjani ilikuwa kati ya Serena Williams na Maria Sharapova ambapo Serena aliendelea kuweka rekodi yake nzuri kwenye mchezo huo kwa kuibuka mshindi.
.
Serena Williams na Maria Sharapova.
.
Serena na Venus Williams. Hapa ilikuwa ni siku za nyuma walipokutana kwenye michuano ya Tennis
TENNIS-OPEN-AUS-FINAL

Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com