Friday, January 30, 2015

DAVIDO NA VIDEO YAKE KALI, JE , UNAWEZA KUMTAMBUA HAPA

 Davido ametusogezea  video mpya- The Sound

.
.
Staa wa Nigeria David Adedeji Adeleke aka Davido time amekuletea video ya single mpya inayoitwa The Sound akiwa amewashirikisha Dj Buckz pamoja na kundi la Uhuru kutokaea Afrika Kusini.


Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

MSANII WA GOSPEL PALE ANAPOMTAJA MSANII ANAEMKUBALI

Pale ambapo Rose Muhando anamtaja msanii wa bongofleva anaemkubali.

Rose MuhandoSio zile stori ambazo tumezoea kuzisoma au kuziona kwenye hii mitandao ambayo tunapita kila siku…. lazima uwe na hamu ya kujua jibu lake iwapo staa wa gospel kama Rose Muhando ataulizwa anamkubali msanii gani wa bongofleva?
Kikawaida siku zote msanii huyu wa bongofleva husifika kwa kufanya show kali sana, yani akiwa kwenye stage hata kama huzijui nyimbo zake lazima ataweza kukuteka tu ambapo haya maneno ya Rose Muhando yalifata baada ya mkali huyu kupiga show Singida kwenye miaka 10 ya Waziri Lazaro Nyalandu ambae pia ni Mbunge Singida.

Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupiti,www.tangakumekucha.blogspot.com

BABA P SQUARE AZIKWA KIFALME NIGERIA

Baba yao P Square alifariki Nov 2014, kazikwa hivi ja Jan 30 2015

Psq VIIMzee Moses Okoye, baba mzazi wa mastaa wa muziki kutoka Nigeria, Peter na Paul Okoye wa kundia laP Square’ alifariki November 25 2014 baada ya kuanguka kwenye ngazi ndani ya nyumba.
Taarifa za wanafamilia zilisema mzee huyo alifanyiwa upasuaji wa goti siku za nyuma na hali yake ilianza kuwa sawa kabla ya kufariki ambapo jana January 30, 2015 ndio mzee huyu amezikwa ikiwa ni miaka miwili imepita toka kufariki kwa mama yao.
Hizi ni picha za safari ya mwisho ya Mzee Moses Okoye, baba wa mastaa mzazi wa P Square na Jude ‘Engees’ Okoye.
Ps
Psq II
PSq Iv
Psq IX
.
Peter na Paul Okoye.
Psq VI
PSQ vkas
.
Peter na kaka yake Jude Okoye.
pSQ
P S 1
PS 2
PS 3
Kulikua na ulinzi pia
Kulikua na ulinzi pia
ps 5
ps 6
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupiti,www.tangakumekucha.blogspot.com

MTOTO WA BECKHAM NDANI YA ARSENAL

Mcheki mtoto wa Beckham ndani ya Club ya Arsenal.

brooklyn
Pamoja na kua mtoto wa nyota wa zamani wa Manchester United, David Beckham kijana Brooklyn Beckham yuko njiani kuanza maisha kama mchezaji wa kikosi cha kwanza cha wapinzani wakubwa wa baba yake Arsenal ‘The Gunners’.
Kijana huyu mwenye umri wa miaka 15 anafahamika kama shabiki wa Arsenal kwa muda mrefu na alisaini kuichezea timu hiyo mwaka jana akianzia kwenye kikosi cha wachezaji wenye umri chini ya miaka 16.
Hivi karibuni Brooklyn alipakia picha kwenye mtandao wa Instagram akiwa na wachezaji wenzie akiwa kwenye vyumba vya kubadilishia nguo vya uwanja wa mazoezi wa Arsenal.
Akiwa amekaa kwenye chumba hicho na wachezaji wenzie Beckham alionekana akiwa mwenye furaha kuwa na wachezaji wenzie na dalili zote zinaonyesha kuwa huenda atafuata nyayo za baba yake ambaye ni moja kati ya wachezaji waliopata mafanikio makubwa kwenye mchezo wa soka.
Brooklyn Beckham akiwa na wachezaji wenzie wa kikosi cha wachezaji wenye umri chini ya miaka 16 wa Arsenal.
Brooklyn Beckham akiwa na wachezaji wenzie wa kikosi cha wachezaji wenye umri chini ya miaka 16 wa Arsenal.
Brooklyn huko nyuma amewahi kufanya majaribio na timu za Chelsea, Manchester United, Fulham na Queens Park Rangers na alifanya majaribio na Arsenal ambao wamemsainisha mkataba tangu mwezi mwezi novemba mwaka jana.
Cha kushangaza kuhusu familia ya Beckham ni kwamba watto wake wote wa kiume ni mashabiki wa Arsenal na hakuna yoyote aliyechagua kufuata nyayo za baba yao ambaye ni shabiki na gwiji wa Manchester United.
Beckham akiwa na Brooklyn wakitoka kuangalia mechi uwanjani huko England .
Beckham akiwa na Brooklyn wakitoka kuangalia mechi uwanjani huko England.
Sio kushabikia tu bali watoto hawa wamekwenda mpaka hatua ya kujiunga na timu hiyo ambapo Cruz mwenye umri wa miaka 9 anachezea kikosi cha vijana wa Arsenal chini ya miaka 10 na Romeo mwenye umri wa miaka 12 anachezea kikosi cha The Gunners kwa watoto chini ya miaka 13 na kaka yao Brooklyn anachezea kikosi cha vijana chini ya miaka 16.
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumecha.blogspot.com

LUIS FIGO NA URAIS WAFIFA

Figo katika harakati za kuusogelea Urais wa FIFA

1224
Wagombea wawili wa nafasi ya Urais kwenye uchaguzi mkuu wa FIFA, Luis Figo na Prince Ali Bin Al Hussein wametangaza kupita hatua ya kwanza ya kuelekea kwenye uchaguzi huo .
Haua hiyo inahusisha kuteuliwa kwa kutiliwa saini na vyama vitano vya soka toka kwenye nchi wanachama wa fifa .
Mchezaji wa zamani wa Ureno na klabu za Sporting Lisbon, FC Barcelona, Real Madrid na Inter Milan, Luis Figo na Rais wa chama cha soka cha Jordan ambaye pia ni makamu wa rais wa FIFA,  Prince Ali Bin Al Hussein ni moja kati ya watu sita ambao hadi sasa wametangaza dhamira ya wazi ya kuingia kwenye mbio hizo za kuwania urais wa FIFA.
Luis Figo amekidhi moja ya vigezo muhimu vya kugombea urais wa Fifa baada ya kuidhinishwa na vyama vitano vya soka toka barani ulaya .
Luis Figo amekidhi moja ya vigezo muhimu vya kugombea urais wa FIFA baada ya kuidhinishwa na vyama vitano vya soka toka barani Ulaya.
Moja ya vigezo vya kuingia kwenye mbio za urais wa FIFA ni kwa kila mgombea kuwasilisha barua zilizotiwa saini na vyama vya soka vya mataifa angalau matano na mpaka kufikia hii leo (Alhamisi) tayari Figo na mtoto wa Mfalme wa Jordan walikuwa wametimiza kigezo hicho.
Inaaminika kua vyama vya soka vya Denmark, Ureno, Montenegro, Macedonia, Luxembourg na Poland ndio vyama vilivyompitisha Figo.
Kwa upande wake Prince Ali alithibitisha kupitia kwenye kigezo hicho ambapo alitumia ukurasa wake binafasi wa Twitter kuwaeleza watu wake kuwa tayari amepata saini za vyama vitano.
Prince Ali Bin Al Hussein naye amepata idhini toka kwa vyama vitano vya soka .
Prince Ali Bin Al Hussein.
Hadi sasa ukiachilia mbali Figo na Pirnce Ali wagombea wengine waliojitokeza ni mchezaji wa zamani wa Ufaransa  David Ginola, kiongozi wa zamani wa FIFA Jerome Champagne, rais wa chama cha soka cha Uholanzi, Michel Van Praag pamoja na rais wa sasa, Sepp Blatter.
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

WAARABU WA PEMBA WAJUANA KWA VILEMBA

Mtazame Mke wa Star wa Real Madrid akiwa uwanjani…

james no 10
Siku zote waarabu wa Pemba hufahamiana kwa vilemba na ndege wa mabawa ya kufana hupaa pamoja , msemo huu unaonekana kuwa kweli kwa familia ya nyota wa Real Madrid na timu ya taifa ya Colombia, James Rodriguez ambaye hivi karibuni alionekana akiwa kwenye uwanja wa mchezo wa Volleyball  akiwa anamtazama mke wake.
Mke wa James Rodriguez ambaye anaitwa Daniella Ospinna ni mchezaji wa timu ya Real Madrid ya mchezo wa  Volleyball na James siku za hivi karibuni ameonekana akiwa kwenye uwanja kumtazama mkewe.
Daniella kama ilivyo kwa mumewe anavaa jezi nambari 10 katika timu hiyo ya Real Madrid na ameonekana kuwa mchezaji muhimu sana hasa kutokana na urefu wake ambao ni kitu muhimu kwa mchezo wa Volleyball hasa kwa mchezaji wa kati.
James Rodriguez akiwa anamtazama mkewe akiwa uwanjani huku akiwa amembeba  mtoto wao .
James Rodriguez akiwa anamtazama mkewe akiwa uwanjani huku akiwa amembeba mtoto wao.
Rodriguez ambaye alisajiliwa na Real Madrid akitokea AS Monaco baada ya kufanya vizuri kwenye michuano ya kombe la dunia amezidi kufanya vizuri akiwa na timu yake mpya ambayo hadi sasa ameifungia mabao 10 kwenye mechi 30 ambazo amecheza kwenye michuano mbalimbali na siku hadi siku umuhimu wake unazidi kuongezeka.
Daniella Ospina akiwa uwanjani anakoiwakilisha klabu ya Real Madrid ya mchezo wa Beach Voleyball.
Daniella Ospina akiwa uwanjani anakoiwakilisha klabu ya Real Madrid ya mchezo wa  Voleyball.
Daniella Ospinna anatokeo kwenye familia ya michezo ambapo ana undugu wa damu na kipa namba moja wa Colombia maybe pia huichezea Arsenal, David Ospinna na kipa huyo ndio hasa alimkutanisha dada yake na James Rodriguez ambaye ni rafiki yake wa muda mrefu na urafiki huo sasa umekuwa undugu ambapo wawili hao sasa wanaitana shemeji.
daniela ospina
danielaaa
rodriguezzz
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

CHALSEA YAPATA PIGO

Pigo Chelsea! Hii ndio adhabu iliyomkuta Diego Costa leo hii

251FF2A400000578-2928837-image-m-32_1422393230347Masaa takribani 24 kabla ya klabu ya Chelsea kuwakaribisha mabingwa watetezi wa Barclays Premier League Manchester City katika dimba lao la Stamford Bridge katika mchezo muhimu wa ligi kuu ya England – vijana wa Jose Mourinho wamepata pigo zito katika kikosi chao.
Mshambuliaji wao tegemeo ambaye ameshafunga magoli 17 kwenye ligi mpaka sasa, Diego Costa amefungiwa mechi 3 kwa kosa la kumkanyaga makusudi mchezaji wa Liverpool Emre Can.
Costa mwenye umri wa miaka 26 atakosa mechi ya wikendi dhidi ya Mancity pamoja na mechi dhidi ya Aston Villa na Everton.
Shtaka hilo ambalo Costa alilikana linatokana na tukio lake alilofanya kwenye mchezo wa kombe la Capital One Cup ambapo Chelsea iliibuka kidedea.
Costa aliyesajiliwa kwa kitita cha pauni millioni 32 ana mabao 17 katika mechi 19 za ligi ya Uingereza msimu huu.

MUGABE APEWA SHAVU AU

Hii ni nafasi nyingine ya uongozi kwa Rais Mugabe

mugabeRais mkongwe wa Zimbabwe Robert Mugabe, ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa Muungano wa Afrika AU akichukua nafasi ya Mohamed Ould Abdel Aziz wa Mauritania.
Mugabe mwenye umri wa miaka 90 ameteuliwa kwa kauli moja na Wajumbe katika mkutano wa AU unaoendelea kwa sasa mjini Addis Ababa-Ethiopia.
Imeelezwa kuwa uteuzi wa Mugabe kuongoza muungano huo mkubwa ulio na wanachama zaidi ya arobaini, huenda ukaleta doa ndani ya AU, kwa kuwa Mugabe hana uhusiano mzuri na mataifa ya Magharibi, hasa baada ya kukaa madarakani tangu Zimbabwe ilipojipatia uhuru mwaka 1980.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

STAA WA BARCELONA AFURAHIA KUPATA MTOTO KIUME

Habari njema kwa familia ya Shakira na mpenzi wake Gerard Pique

EXCLUSIVE: Shakira and Gerard Pique strolling with baby Milan in SpainFamilia ya mwanasoka mahiri Gerard Pique na mkewe Shakira wamepata ugeni mpya ndani ya familia hiyo baada ya mwanamuziki huyo kujifungua mtoto wa pili wa kiume.
bal
Mtoto huyo aliyepewa jina la Sasha likiwa na maana ya Alexander kwa lugha ya Kirussia, alizaliwa katika hospitali iliyopo katika mji wa Barcelona usiku wa kuamkia leo kwa njia ya upasuaji.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

BABA AJIUA BAADA YA KUONA PICHA A UTUPU ZA BINTI YAKE

Binti huyu alipiga picha na kusambaza kwenye mitandao ya kijamii, baada ya hapo ni Stori!

 
loreWazazi wamekua na nafasi kubwa sana katika malezi ya watoto wao hata wakati pale wanapokuwa watu wazima lakini baba huyu kutokana na upendo kwa mwanaye aliamua kujiua baada ya kuona picha za mtoto wake alizopiga akiwa mtupu katika jarida la Playboy nchini Romania.
Loredana Chivu anayeishialiamua kuweka picha hizo akiwa amepiga katika staili tofauti katika mitandao mbalimbali ya kijamii ambapo baba yake baada ya kuziona alimkana mwanaye huyo.
lore2
Loredana Chivu msichana aliyesababisha kifo cha baba yake
Kwa mujibu wa mtandao wa The Mirror, msichana huyo akisimulia kwa machungu baada ya kifo cha baba yake alisema hakutegemea kama ipo siku baba yake angekasirika kiasi cha kujitoa uhai.
Kutokana na maadilili picha hizo hatutaziweka picha hizo
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

D' BANJ AFUNGUKA

Miaka 10 ya D’Banj kwenye muziki anajivunia mafanikio makubwa! kuhusu NDOA je?…

DBA
Mkali wa Nigeria D’Banj amefunguka na kusema amekuwa mmoja wa mastaa wakubwa katika Industry ya muziki ambaye bado hajaoa na sasa amevunja ukimya na kutamka kuwa ana mpango ya kupata mtoto mwaka huu pamoja na kufunga ndoa.
D’Banj ambaye kwa sasa amefikisha miaka 35 alisema mwaka jana alilazimika kuoa baada ya mama yake kumsisitiza lakini alikua hajajiandaa vya kutosha lakini sasa anaweza kutekeleza nia yake hiyo .
Sijajua itakua lini rasmi…lakini nafikiri kufanya yote mwaka huu,kila siku nimetamani kupata mtoto”:-D’Banj
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

MKASA WA MZAZI KUWAFUKIA WATOTO WAKE WA KUWAZAA

MKASA MZIMA WA YULE MAMA ALIYEWANYONGA WATOTO WAKE WAWILI WA KUWAZAA KISHA KUWAFUKIA NDANI YA CHUMBA CHAKE

BADO hali ni tete kufuatia mwanamke mmoja, Zuhura Sudi (26), mkazi wa Mtaa wa Utusi Kata ya Chemchemi Manispaa ya Tabora kudaiwa kuwaua kwa kuwakaba shingo watoto wake wawili, Mwamvua (6) na Sudi Mrisho (miezi saba) kisha kuwazika kwenye mashimo mawili ndani ya nyumba.

Mwanamke (Zuhura Sudi) anayetuhumiwa kuwaua watoto wake.
Tukio hilo ambalo limeishangaza nchi hasa kufanywa na mama mzazi ambaye anaujua uchungu wa kuzaa, lilijiri Jumapili usiku ndani ndani ya nyumba ya mwanamke huyo.
SIKU MOJA KABLA
Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari vya uhakika, siku moja kabla ya tukio, mwanamke huyo ambaye ni mtata kiasili alionekana akicheza na watoto wake na watoto wa jirani huku akionesha uchangamfu mkubwa.
“Kama wale watoto wake wangejua mama yao mzazi ndiyo safari ya kifo chao naamini wasingemchangamkia mama yao.
“Walicheza kwa amani, kwa upendo. Kumbe mama ana mahesabu yake. Haiwezekani leo niambiwe kuwa mawazo ya kuwaua watoto wake aliyapata ghafla,” alisema shuhuda mmoja.
Mtuhumiwa akiwa chini ya ulinzi.
USIKU, JIRANI ASIKIA KISHINDO
Jirani mmoja na nyumba ilipotokea tukio alisema:
“Mimi awali ya siku ya kuelekea usiku wa tukio, nilimwona yule mama. Nikasalimiana naye. Alionekana yupo kawaida tu.
“Lakini usiku, kukiwa kumetulia nilisikia vishindo kama mtu anachimba ardhi. Nilipofuatilia nikabaini vilikuwa vikitoka upande wa nyumbani kwa mwanamke yule.“Sikushtuka. Nilijua ni shughuli zake za  kawaida zinaendelea ndani ya nyumba yake. Kulipokucha sasa, nikasikia yule mama anasema kwamba watoto wake wamepotea.
“Palepale nikaanza kuhisi kitu kwa ile mishindo ya usiku. Inaonekana alishawaua watoto wake sasa alikuwa anachimba mashimo ya kuwafukia. Kule si kuwazika na yale si makaburi ni mashimo. 
“Inauma sana, siamini kama mama aliyezaa watoto kwa uchungu mkubwa anaweza kufanya ukatili kama huu.”
Miili ya watoto hao baada ya kufukuliwa kwenye mashimo.
AKILI ILIMWAMBIA ASUBIRI AKIWA PEKE YAKE
Baadhi ya majirani walisema ndani ya nyumba hiyo kuna watu wengine wanaishi, lakini mtuhumiwa huyo alisubiri akiwa peke yake ndipo akatekeleza ukatili wake wa kutisha.
ANACHOJUA MWENYEKITI WA MTAA
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Mtaa wa Utusi, Aziza  Mwenya, ushirikiano mkubwa  kati ya  wananchi  wa mtaa  huo  ndiyo uliofanikisha  kugundulika  kwa tukio  hilo  la  kinyama  lililopoteza  maisha  ya  watoto  hao  wasiokuwa na hatia.
“Baada  ya  kupokea taarifa  kutoka  kwa  babu  wa  Zuhura, mzee Shaban Ramadhan kuhusu  kutoweka  kwa watoto  hao katika  mazingira ya kutatanisha, tulifika  kwenye nyumba ya tukio kwanza na kumhoji  mama wa watoto.
Ndugu na majirani wakiwa na makamanda wa Polisi eneo la tukio.
“Cha ajabu  alikuwa akizuia watu  kuingia ndani. Kumbe alishajua kinachoendelea na akiruhusu sisi kuingia nini kitatokea.“Hata hivyo majirani kwa kushirikiana na mimi na baba wa mmoja wa watoto waliouawa (Sudi Mrisho), Mrisho Abdallah tulimshika kwa nguvu  Zuhura, watu wakaingia.”
WAKUTA MASHIMO MAWILI
“Tulipofika, tukabaini mashimo mawili aliyokuwa amewafukia watoto wake. Shimo moja sebuleni, jingine chumbani. Tuliwapa taarifa polisi wakafika haraka sana. Mashimo yalipofukuliwa, watoto walikutwa ndani ya mifuko miwli ya sandarusi. Inauma sana. ”
MTUHUMIWA AZUNGUMZA NA AMANI
Amani lilibahatika kuzungumza na mwanamke huyo katika mahojiano mafupi akiwa chumbani muda mfupi kabla ya polisi kufika.Amani: “Hivi Zuhura, ni kwanini umeamua kuwaua watoto wako wa kuwazaa?”
Zuhura: “Nani? Mimi sijui, we (mwandishi) ndiyo unajua.”Amani: “Watoto wako wako wapi?”
Zuhura: “Nani? Wako wapi kwani?”
KILICHOONEKANA
Baadhi ya wakazi wa eneo hilo walisema, Zuhura licha ya kuonekana hana wasiwasi wowote, lakini pia aliashiria kujitoa ufahamu ili atafsirike kwamba hakuwa na akili timamu.
KUMBUKUMBU MBAYA
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa majirani zinadai kuwa, mwaka 2013, Zuhura alidaiwa kumsababishia kifo mtoto wake mchanga  wa kiume kufuatia kumzidishia dozi ya malaria wakati alipokuwa akiumwa.
KAMANDA WA POLISI
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora,  ACP Juma Bwire ilikiri kutokea kwa tukio hilo.
Afande Bwire alisema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
 
   Chanzo habari na matukio
 

TETESI ZA USAJILI ULAYA , MAN YASHIKWA NA KIGUGUMIZI KWA BEKI HUYO

Huyu ndio beki ambaye Man United wamegoma kukanusha kutaka kumsajili

2501322500000578-2931379-image-a-51_1422537948921Dirisha la usajili barani ulaya limebakiza takribani masaa 48 kabla ya kufungwa, na kama ilivyo ada tetesi za usajili wa wachezaji tofauti zimezidi kushika kasi.
Klabu ya Manchester United ambayo imekuwa na udhaifu kwenye kikosi hasa kwenye maeneo ya kiungo na beki wa kati, leo hii Manchester United wameshindwa kukanusha taarifa kwamba wametuma ofa ya £37m kwa Borussia Dortmund na kuanza mazungumzo kwa ajili ya usajili wa beki  Mats Hummels. Inaaminika ikiwa usajili huo utafanikiwa basi beki wa Dinamo Kiev Aleksandar Dragovic atanunuliwa kurithi mikoba ya Hummels.
United wamekuwa wakihusishwa na usajili wa Mats Hummels tangu wakati wa dirisha la kiangazi lakini walikutana na kizingiti cha Dortmund kugoma kumuuza beki huyo mshindi wa kombe la dunia mwaka 2014, lakini sasa klabu hiyo ambayo ipo kwenye mkia wa msimamo wa Bundesliga inaonekana kuwa tayari kumuuza beki huyo ambaye pia alikuwa akihusishwa na kutakiwa na Arsenal.
Wakati huo huo mchezaji na nahodha msaidizi wa Man United Darren Fletcher anatarajiwa kujiunga na West Ham United kwa uhamisho wa bure na anategemewa kusaini mkataba wa miaka miwili na nusu ikiwa kila kitu kitaenda kama kilivyopangwa.

KANYE WEST ANAKUJA NA KIBAO KIPYA AKIMSHIRIKISHA MTOTO WAKE MCHANGA

Kanye West amekuja na  video ‘Only one’ ndani yumo mtoto wake North

norrrRapa Kanye West  ameamua kumpa shavu mtoto wake North West katika video mpya ya ‘Only one‘ aliyomshirikisha Paul MacCartney.

Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

KUNA NCHI ZAPIGA MARUFUKU WATOTO KUPEWA MAJINA YASIOENDANA NA TAIFA LAO

Unajua kuna nchi zinapiga marufuku watoto kupewa baadhi ya majina? Yako hapa…

sad-kid
Huku kwetu tuna utaratibu wa kuwapa watoto wetu majina tunayopenda, yapo majina ya watu maarufu kama viongozi, wanasoka, waigizaji na wengineo.
Kuna hizi nchi ambacho wao wamepiga marufuku baadhi ya majina kupewa watoto, list ni hii hapa.
New Zealand: Msajili wa Vizazi, Vifo na Ndoa nchi hii ameagiza baadhi ya majina kupigwa marufuku ikiwemo majina haya; Majesty, Queen Victoria, Lucifer na jina la Mafia No Fear.
VenezuelaWao wamezuia matumizi ya jina la Superman kwa kuwa ni gumu kulitamka.
Denmark: Wametoa list ya majina rasmi ambayo yako zaidi ya 7,000 mtoto akizaliwa anachaguliwa jina kati ya majina hayo, moja ya majina yaliyozuiwa huku ni jina la Monkey.
Brazil: Jina lililozuiwa huku ni jina la Saddam Hussein.
Mexico: Wamepiga marufuku mtoto kupewa majina ya Scrotum, Terminator, Burger King, Hitler na Virgin.
Uturuki: Mahakama imezuia mtoto kupewa jina la Osama Bin Laden
Portugal: Wao wamezuia jina la Tom.
Mfano hii ingekuja Bongo, majina gani ungependa yazuiwe wasipewe watoto wetu?
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia, www.tangakumekucha.blogspot.com

SOMA HABARI KUU ZILIZOPEWA UZITO MAGAZETI YA LEO,TZ

Soma stori  zilizopewa uzito kwenye Magazeti ya leo Tanzania January 30, 2015, nimekuwekea hapa

roun
MTANZANIA
Taarifa ya mwaka ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), ya hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu na mashirika ya umma kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2013, imebua wizi wa kutisha wa fedha za umma uliofanywa na taasisi hizo.
Hayo yalibainika jana wakati Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe, alipokuwa akiwasilisha ripoti ya kamati hiyo, ambapo alisema katika ripoti za ukaguzi kwa Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL), imebainika kuwa ililipa mabilioni ya fedha kwa ajili ya ndege iliyoikodi kutoka Shirika la Ndege la Wallis Trading Inc la China, ndege ambayo ni hewa kwa kuwa haipo nchini.
Hadi sasa Serikali imelipa dola za Marekani 26,115,428.75, (Sh bilioni 45.17) na sasa inadaiwa dola za Marekani 23,996,327.82 (Sh bilioni 41.51), ndege hiyo ilikuwa mbovu na ilifanya kazi nchini kwa miezi sita pekee badala ya miaka sita kama mkataba wa ubinafsishwaji ulivyotaka:-Zitto.
Taarifa hiyo ya PAC, ilibainisha pia kuwa katika ujenzi wa jengo la watu mashuhuri (VIP) katika Uwanja Ndege wa Kimatifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, kuna ufisadi wa takriban Sh bilioni tisa.
Ilisema pia jengo hilo lilianza kujengwa bila kibali cha Baraza la Mawaziri na kuwa thamani ya gharama za ujenzi wa jengo hilo hazijulikani kwa kuwa nyaraka muhimu hazipo.
Kwa upande wa Mamlaka ya Bandari (TPA), imebainika kutumia Sh bilioni 9.6 kwa ajili ya vikao vya wafanyakazi na mamilioni mengine kujilipa kwa ajili ya posho za safari bila kuwa na kibali kutoka serikalini.
Zitto alisema pia kamati yake imebaini kuwa misamaha ya kodi imezidi kuongezeka na kufikia Sh trilioni 1.8 mwaka 2014, huku zaidi ya Sh bilioni 80.45 za misamaha hiyo kwa mwaka zikitumika kwa njia zisizo halali.
NIPASHE
Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), imepoteza Sh. bilioni sita katika ujenzi wa gati kwenye Ziwa Tanganyika kutokana na kila mkandarasi anayepewa kazi hiyo kuingia ‘mitini’ kabla ya kumaliza kazi hiyo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Madeni Kipande, alimweleza Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, wakati akielezea hali ya utendaji kazi wa mamlaka hiyo alipofanya ziara juzi.
Alisema kumekuwa na changamoto nyingi katika utekelezaji wa miradi ukiwamo ujenzi wa gati Ziwa Tanganyika na Bandari ya mwambani mkoani Tanga.
Kipande alisema mfano katika utekelezaji wa ujenzi wa bandari ya Mwambani Tanga, kampuni 34 zilinunua vitabu kwa ajili ya kuomba zabuni ya ujenzi wa bandari hiyo lakini hadi inafika mwisho wa kurudisha vitabu hakuna hata kampuni moja iliyorudisha.
Kuhusu wizi bandarini, aliiomba serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi kusaidia kuwabana mawakala wa mizigo bandarini kwa kutumia sheria iliyopo kwa kuwa wamekuwa mawakala wa wezi.
Alisema mawakala hao wamekuwa wakiwabambikizia bili wateja na kwamba kuna haja kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuweka bei zinazolingana ili wateja wasiwe wanabambikiziwa bili.
NIPASHE
Sakata la kupigwa na kudhalilishwa kwa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba na wafuasi wengine wa chama hicho, limeibua mapya, baada wabunge wa upinzani kuja juu wakitaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe wawajibike au Bunge liwawajibishe.
Wengine, ambao wabunge wanataka wawajibike ni Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali (IGP), Ernest Mangu, naibu wake (DIGP), Abdukrahman Kaniki, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa jeshi hilo, Paul Chagonja pamoja na wote waliohusika na kadhia hiyo.
Pia wametaka viongozi wengine wa polisi waliohusika ama kutoa amri au kutekeleza unyama huo wachukuliwe hatua za kisheria na jeshi hilo lifumuliwe na kuundwa upya.
Walisema hayo kwa nyakati tofauti wakati wakichangia bungeni mjadala kuhusu hoja iliyohusu jambo la dharura, iliyotolewa na Mbunge wa Kuteuliwa (NCCR-Mageuzi), James Mbatia na kauli ya serikali, kuhusiana na yaliyotokea Januari 27, mwaka huu, Mbagala, jijini Dar es Salaam.
Katika mjadala huo, Waziri Chikawe pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), George Masaju, walipatwa na wakati mgumu wakijaribu ama kutoa hoja za kuzuia mjadala kuhusu suala hilo kufanyika bungeni au kuwatetea polisi na kumkandamiza Prof. Lipumba.
NIPASHE
Watu watatu wametiwa mbaroni kwa tuhuma za kuhifadhi na kuuza sigara za magendo maeneo ya Mbagala jijini Dar es Salaam kwa lengo la kukwepa kulipa kodi.
Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Siro, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Efeso Tweve, Omary Metson na Frank Mrema.
Alisema operesheni hiyo iliendeshwa na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Biashara hiyo ya magendo ilianza kushamiri tangu mwaka 2012 kutokana na serikali kutoza kodi kubwa kwa bidhaa ya sigara na inakadiriwa kuwa asilimia nne ya sigara zote zinazouzwa Tanzania, ni za magendo.
Sigara hizi zinatengenezwa Tanzania kihalali kabisa kwa  ajili ya kuuzwa nchi za nje, lakini baadhi ya wafanyabiashara walioko kwenye mtandao wa bidhaa za magendo huzirudisha nchini bila kulipia kodi:-Siro.
Aidha, serikali hupoteza wastani wa Sh. bilioni 10 kila mwaka kama kodi kutokana na biashara hiyo ya magendo na kwamba kwa sasa kodi za Tanzania kwa sigara inafikia asilimia 36 ya bei za reja reja za bidhaa hiyo.
MWANANCHI
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda amevipa siku 14 viwanda vinavyozalisha bidhaa zilizo chini ya kiwango kuziondoa sokoni sambamba na kuujulisha umma namna watakavyoziharibu na kuziteketeza.
Waziri Dk Kigoda alitoa amri kwa kampuni tatu kuondoa bidhaa zake sokoni baada ya kugundulika kuzalishwa chini ya kiwango na kusisitiza kuchukua hatua kali za kisheria kwa yeyote atakayekaidi agizo hilo.
Kupitia taarifa kwa umma iliyochapishwa jana, Waziri Kigoda alisema kampuni hizo zinatakiwa kutekeleza agizo hilo na kutoa taarifa ya utekelezaji kwa Shirika la Viwango la Taifa (TBS).
Kampuni zilizobainika kuzalisha bidhaa zilizo chini ya viwango ni pamoja na Kiwanda cha Devideic Group Ltd kinachotengeneza maji ya matunda aina ya Into, Ufresh Limited cha Tegeta kinachozalisha juisi aina ya Ufresh na Kampuni ya Kutengeneza Chumvi ya Sea Salt.
Ofisa Mdhibiti wa TBS, Deusdedit Paschal alisema chumvi inayozalishwa na kiwanda hicho ina madini joto ya miligramu 14.9 pekee wakati kiafya chumvi hutakiwa kuwa na miligramu 30-60.
MWANANCHI
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema kama Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) itaona muda wa uandikishaji wananchi katika Daftari la Wapigakura kwa ajili ya Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa hautoshi, atawasilisha suala hilo bungeni ili uongezwe.
Pinda alisema hayo bungeni mjini Dodoma jana katika kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu bungeni alipokuwa akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe aliyemtaka kueleza Serikali ina mpango gani kuhakikisha hakuna tatizo litakalotokea katika uandikishaji, hasa ikizingatiwa kuwa muda uliopo hautoshi na majaribio ya uandikishaji kwa BVR umeibua kasoro nyingi.
Akijibu swali hilo, Pinda alisema: “Aliyoyasema Mbowe, Serikali haiwezi kuyapuuza hata kidogo na ni kweli mchakato huo umekuwa na matatizo kidogo hasa ya fedha na Serikali imekuwa ikipambana ili kuweza kufanikisha mchakato huo,” alisema Pinda.
Jana, Mbowe alisema majaribio ya uandikishaji wa kutumia mashine za kielektroniki za BVR katika majimbo ya Kawe, Wilaya ya Mlele na Kilombero yameibuka na changamoto mbalimbali na huku nchi ikitakiwa kuandikisha wapigakura zaidi ya milioni 24 na kuhoji kuhusu muda uliopangwa wa uandikishaji, hasa ikizingatiwa kuwa zimebaki siku 90 kufikia kwenye kura ya maoni huku mashine moja ikiwa na uwezo wa kuandikisha watu 22 kwa siku.
MWANANCHI
Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro linamshikilia mwalimu mmoja wa shule ya sekondari kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa kidato cha tatu na kumuumiza sehemu za siri.
Kamanda Koka Moita alisema mwalimu huyo alimwita mwanafunzi huyo katika chumba hicho na kuanza kumtomasa mwilini na baadaye alimvua nguo kwa nguvu, kisha kumuingilia.
Alisema kutokana na maumivu aliyoyapata alipelekwa Hospitali ya Mkoa ya Mawenzi kwa matibabu. Kamanda Moita alisema mtuhumiwa baada ya kutenda kosa hilo alikamatwa.
JAMBOLEO
Watu wasiojulika wamevamia ofisi ya muhasibu katika shule ya St.Christina  ya Jimbo katoliki Tanga  iliyopo kata ya Maweni na kuiba shilingi milioni 126 kisha kuichoma ofisi hiyo kwa lengo la kupoteza ushahidi.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo,kaimu kamanda wa Mkoa wa Tanga, Juma Ndaki alisema miongoni mwa fedha zilizoibwa ni karo za wanafunzi ambapo hadi sasa jeshi la polisi linamshikilia mlinzi na wenzake watano ambao wanatiliwa shaka.
Ndaki alisema upelelezi unaendelea kufanyika ili kuwabaini wahusika wa tukio hilo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blogspot.com

Thursday, January 29, 2015

AMKA NA MAGAZETI NA KUMEKUCHABLOG

MAGAZETI YA LEO,30/01/15 YANALETWA KWA HISANI YA MKOMBOZI SANITARIUM CLINI, MABINGWA WA MAGONJWA SUGU, WAPO CHUDA TANGA, SIMU 0654 361333