Saturday, August 8, 2015

NILIJUA NIMEUWA SEHEMU YA (6)

HADITHI
 
NILIJUA NIMEUA (6)
 
ILIPOISHIA
 
“Wafukuze wapangaji wote halafu uikarabati hii nyumba” nikamwambia.
 
“Unataka tuishi peke yetu?”
 
“Ndiyo. Sitaki kero. Chumba kimoja uweke sebule”
 
“Kwa vile nakupenda nitafanya hivyo”
 
Baada ya wiki moja nikaufanyia kazi ushauri wa Halima. Niliwapa notisi wapangaji wote, nikaikarabati nyumba na kuweka chumba kimoja kama sebule.
 
Nilikuwa na shamba langu la minazi. Fedha nilizopata kutokana na mauzo ya nazi zilinisaidia sana kukamilisha nyumba yangu.
 
Halima aliendelea kunitembelea mara kwa mara. Alipohakikisha nimetimiza matakwa yake akanielekeza kwa wazazi wake nipeleke barua ya uchumba.
 
Wazazi wa Halima walikuwa wakishi Pongwe, mwendo wa karibu kilometa kumi na tano kutoka Tanga mjini. Baba yake Halima mzee Moto Bwagizo alikuwa mtu mzima sana. Niliambiwa kuwa Halima alikuwa mtoto wake wa mwisho na alizaliwa bila kutegemewa kwani tayari baba yake alikuwa mzee. Mama yake mzazi alishafariki.
 
SASA ENDELEA
 
Mzee Moto Bwagizo alikuwa na wake wawili, mama yake Halima na mke mwingine. Baada ya kufariki mama yake Halima, mzee Moto aliendelea kuishi na mke wake wa pili.
 
Niliwasilisha ujumbe wangu kwa wazazi wa Halima. Baba mkwe aliponiona aliniambia hazitambui mila za kutuma barua ya uchumba kwani mimi sikuwa nikiomba kazi. Ukiomba kazi ndio unatuma barua.
 
“Mila ninazizijua mimi za kutpka enzi na enzi ni za kutuma mshenga, anakuja na maneno tu”
 
“Samahani baba yangu, sikujua ndio kama unanielimisha”
 
Mzee akacheka.
 
“Umenijibu vizuri. Sasa fungua barua yako unisomee”
 
Nikafungua ile barua yangu na kumsomea yale niliyoandika.
 
Mzee akafurahi akaniambia.
 
“Nimekuelewa. Unataka kuunga udugu na sisi. Mimi kama baba wa Halima nakujibu hapa hapa kuwa nimekukubali. Halima ni mchumba wako tangu sasa”
 
Mzee Moto alinitajia kiasi cha pesa alichotaka ili aniozeshe binti yake.
 
Siku ya pili yake nilimchukua rafiki yangu nikaenda naye kupeleka pesa hizo.
 
Mipango ya harusi ikafanywa.
 
Baada ya wiki mbili nikaenda Ponwe kumuoa Halima.
 
Baada ya kuoana na Amina ndipo nilipoanza kufaidi maisha ya ndoa. Kuse,ma kweli yalikuwa matamu kinyume na kuishi kihuni.
 
Kwanza gharama ya maisha ilipungua sana. Pesa ambayo hapo mwanzo nilitumia peke yangu kwa siku  kwa kula kwenye mikahawa, ilitumika kwa siku mbili nilipokuwa na mke wangu.
 
Kadhalika nilikuwa na mwenzangu wa karibu wa kuniliwaza, kunishauri na kunisaidia pale nilipohitaji mwenza wa kunisaidia.
 
Kwa kweli nilihisi raha na nilijilaumu kwa kuchelewa sana kumuoa Halima.
 
Niliendelea na kazi yangu ya teksi. Fedha nilizopata ntulitumia, kiasi kingine tuliwek kama akiba yetu. Miezi michache tu baad ya kuoana, ndoa ilijibu. Halima akapata ujauzito.
 
Halima alinijulisha usiku kuwa alikuwa mjamzito. Wakati tunataka kulala aliniambia.
 
“Subiri”
 
“Nisubiri nini?” nikamuuliza.
 
“Subiri nikuoneshe kitu”
 
“Kitu gani?”
 
“Una haraka gani?”
 
Halima akasimama mbele yangu na kuushika mkono wangu kisha akaushikisha kwenye tumbo lake chini ya kitovu. Akawa anautomasisha kwenye tumbo lake.
 
“Unaona nini?” akaniuliza.
 
“Sioni kitu” nikamjibu.
 
“Huoni kitu kigumu gumu?”
 
“Nakiona, ni nini?”
 
Halima akauachia mkono wangu kisha akapanda kitandani. Wakati anavuta shuka nilimuuliza.
 
“Mbona hukiambii ni nini?”
 
“Mimba!” akanijibu huku akiendelea kijifinika.
 
“Hiyo ni mamba?”
 
Ndiyo”
 
“Mbona ndogo sana?”
 
“Si ndio inaanza, ina mwezi mmoja. Ujue mwezi uliopita sikupata siku zangu”
 
Ni kweli ilikuwa mamba ya mwezi mkmoja. Ilitupa furaha sote wawili. Tukaona karibuni tutaitwa baba na mama.
 
Lakini kadiri siku zilivyoendelea Halima alikuwa akiniambia anapolala usiku anaota ndoto amejifungua watoro wawili mapacha. Watoto hao ni wazuri na weupe kama wazungu!
 
Nikadhani labda ni kweli atajifungua mapacha. Mimba ilipoiza miezi mitatu Halima aliota akifanya tendo la ndoa na mwendawazimu. Alipoamka akaanza kuumwa tumbo!
 
“Una nini?” nikamuuliza nilipomuona akifurukuta.
 
Akanihadithia ile ndoto aliyoota kasha akaniambia alipoamka aliona tumbo linamuuma.
 
Wakati ananieleza hali ilizidi kuwa mbaya. Nikafikiria nimpeleke hospitali lakini ile mamba ikatoka muda ule ule.
 
Sikujua alikuwa amepatwa na tatizo gani. Ilikuwa saa kumi na mbili asubuhi. Nikatoka naye na kumpakia kwenye teksi, tukaenda hospitali ya Bombo.
 
Tulipofika hospitali nilimpigia simu rafiki yangu Dk Augostino Kweka. Kwa bahati njema alikuwa pale pale hospitali, akaja kumtazama mke wangu kisha  akaniambia.
 
“Anahitaji kusafishwa. Mimba haikutoka yote”
 
Dk Kweka alinisaidia sana. Alilichukua jukumu lile kirafiki. Mpaka inafika saa tatu mke wangu alikuwa ameshasafishwa.na kupelekwa wodini. Mimi mwenyewe nilikuwa hapo hapo hospitali muda wote.
Usikose uhiondo huu ni kitajitokeza katika mfululizo huu wa hadithi hii ya kusisimua, hapahapa tangakumekuchablog
 

No comments:

Post a Comment