
Wenger, ambaye anakabiliwa na shinikisho baada ya kushindwa mechi moja pekee kati ya sita walizocheza karibuni amekuwa akitakiwa na baadhi ya mashabiki ajiuzulu.
"Lazima niseme kwamba, licha ya yote yaliyofanywa na baadhi ya mashabiki, mashabiki wetu walikuwa wazuri sana leo," alisema Mfaransa huyo baada ya mechi.
Arsenal, ambao wameshuka hadi nafasi ya sita kwenye Jedwali, walitoka nyuma mara mbili kulazimisha sare hiyo dhidi ya vijana hao wa Pep Guardiola.
"Katika nyakati ngumu sana, tukiwa 1-0 chini na 2-1 chini, wangetugeuka lakini nafikiri walikuwa wazuri sana na walituwezesha kupitia vipindi hivyo vigumu."
BBC
No comments:
Post a Comment