Mike Tyson kumfunza Chris Brown kumpiga Soulja Boy
Nitamfunza vile atauma sikio la mtu," alisema Mike Tyson.
"Nitamfunza kila mbinu chafu. Kwa sababu siwezi kumfunza jinsi ya kukimbia."
Soulja Boy anafunzwa na bingwa mwingine wa ndondi, Floyed Mayweather.
Pigano hilo la raundi tatu litafanyiwa huko Las Vegas tarehe ambayo haijatangazwa.
Wote hao walinza kuchapisha picha na video za kutishana.
Soulja Boy ndiye aliandika kuhusu pigano hilo lakini akaondoa ujumbe huo badaye.
50 Cent amemuanga mkono Soulja Boy na kusema kuwa atatoa dola laki moja kwa matokeo ya pigano hilo.
Chris Brown wa umri wa miaka 27 na Soulja Boy 26, wamekosolewa na wasanii wengine kwa kuzozana hadharani.
Soulja Boy aidha analaumiwa kwa kutumia pigano hilo kama njia ya kufufua taaluma yake ya muziki inayofifia.
BBC
No comments:
Post a Comment