Friday, July 31, 2015
UZINDUZI JEZI MPYA YA SIMBA NA MADUKA YAKE LEO
KIPENGA FOMU ZA URAIS CHAPULIZWA
Hii ndio Ratiba ya Kuchukua Fomu za Urais kwa Wagombea wa Vyama Vyote TZ…
Kwenye maelezo ya Jaji Damian Lubuva Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi >>> “Tunaanza
kutoa Fomu kwa wale wanaogombea urais, kesho (leo) UPDP watakuja kuchukua
fomu saa tatu asubuhi wamesema hawana shamrashamra… TLP wao watakuja saa
sita mchana wanakuja kwa shangwe… DP wao wanakuja saa nane mchana pia
nao wamesema watakuja kwa shangwe pia” >>>>
“Jumanne
August 4 watakuja CCM saa sita mchana watakuja kwa shangwe kama wengine…
Jumatano watakuja ADC saa tatu asubuhi, wao hakuna shamrashamra baada
ya hapo watakuja TADEA saa nne asubuhi pia wao hawana shangwe” >>>>
“August 17 watakuja ACT- Wazalendo saa
tatu asubuhi wanakuja kwa shange pia… muda wa kuandikisha wapigakura kwa
mfumo wa BVR unaisha rasmi tarehe August 8 na baada ya hapo Ratiba ya
Tume itaendeleakuruhusu Uchaguzi Mkuu” >>>> Jaji Damian Lubuva, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi.
MABILIONE 5 LIGI KUU UINGEREZA
Hawa ndio wakali wengine watano Ligi ya Uingereza wenye utajiri mkubwa zaidi, na pichaz zao…
Mastaa wa soka wana utajiri wao wa
kutosha tu, unaambiwa kutokana na kazi nzuri wanayoifanya hata thamani
yao inaongezeka vilevile, ukisikia staa wa soka kanunuliwa kwa pound.
Mil 100 Uingereza basi uwe na jibu kabisa kwamba YES jamaa ni jembe la
kazi !!
Lakini thamani yake haiishii uwanjani,
hata nje ya Uwanja jamaa wa Kampuni kama Nike, PUMA, ADIDAS hawamwachii
apite hivihivi wasimpe hata dili moja eti?
Soka na maisha yao nje ya Uwanja
vinasababisha wajikusanyie pesa na wawe na utajiri wa kutosha kabisa…
karibu uipitie hawa watano ambao wametajwa kuwa na utajiri wa juu zaidi
kwenye List ya mastaa wanaochezea Ligi Kuu Uingereza!!
No.5: Utajiri
wake unakadiriwa kuwa kama Dola Milioni 55, umri wake ni miaka 27 tu
lakini tayari kaonesha Ulimwengu jinsi ambavyo ana uwezo mkubwa Uwanjani
kitu ambacho kimempa thamani ya juu pia kati ya mastaa wa Uingereza…
Jamaa anachezea Klabu ya Manchester City.
No.4: Bastian Schweinsteiger, moja ya Vifaa vya nguvu ambavyo vimeenguliwa kutoka Bayern Munich msimu huu na kujiunga na Man United.. Kama akionesha uwezo zaidi basi huenda akapanda chati na kuuongeza utajiri wake ambao kwa sasa ni kama Dola Mil. 60 hivi.
No.3: Japo umri wake ni mkubwa, miaka 34 lakini hata akisema anastaafu leo Klabu ya Chelsea
itakuwa na heshima kubwa kwake kwa mchango mkubwa alioutoa kwa Klabu
hiyo kwa miaka mingi ambayo ametumia akiichezea Klabu hiyo. Yuko vizuri
pia kwenye nafasi ya tatu akiwa na utajiri wa Dola Mil. 65.
No.2: Yaya Toure ni nafasi ya pili na ndio staa wa Soka pekeake kwenye hii list ya watano ambae ana asili ya Afrika. Utajiri wake ni kama Dola Mil. 75.. Jamaa ni mmoja wa vichwa ambavyo vinategemewa sana Man City.
No.1: Mkali wa Uingereza na mwenyeji wa hapohapo yani.. Kichwa kinachofanya vizuri Manchester United, na ni mmoja ya wakali ambao Uingereza na Man United wanajivunia sana, ukali wake umefanya akae #1 na utajiri wake ni Dola Mil. 110 akimuacha Yaya kwa Dola Mil. 35 hivi !!
AZAM YATINGA NUSU FAINAL
Matokeo ya mechi za nusu fainali, Azam FC katinga fainali? jibu lipo hapa
Nusu fainali ya michuano ya kombe la Kagame
imechezwa July 31 kwa timu nne kushuka dimbani, huku timu mbili pekee
zitakazoshinda ndio zitakazo cheza mchezo wa fainali jumapi ya August 2
Uwanja wa Taifa Dar Es Salaam.
Azam FC imekuwa timu ya pili kutinga fainali baada ya kuifunga klabu ya KCCA ya Uganda kwa goli 1-0 bao pekee lililofungwa na Farid Mussa dakika ya 76. Hivyo Azam FC itacheza mchezo wa fainali na klabu ya Gor Mahia ya Kenye ambayo imeifunga Al Khartoum ya Sudan kwa goli 3-0.
MASTAA WA LIVERPOOL WAKIJINOA
Cheki mastaa wapya wa Liverpool walivyoipania ligi kuu…
Agosti 8 pazia la ligi kuu ya Engaland linafunguliwa rasmi.
Klabu zote zimeonekana kujipanga vyema ili kukabiliana na mikiki ya ligi hiyo, lakini wachezaji wapya wa Liverpool Christian Benteke na kiungo Mbrazil Firmino wameonyesha wamepania kuiletea klau yao mambo mazuri.
Katika mazoezi ya Liverpool, wachezaji hao na wenzao wamekuwa wakifanya kila kitu kwa juhudi na kuonyesha kupanga kuleta mabadiliko makubwa katika kikosi chao ambacho wao ni sura mpya.
Watazame wakiwa kwenye mazoezi yao…
Kwa habari, matukio na michezo, ungana nami hapa hapa tangakumekuchablog
WAKALI KUPEPETANA WEMBLEY
Ngao ya Jamii Ligi Kuu England ni Chelsea Vs Arsenal Jumapili hii,wengine je?..
Kipenga cha kuanza kwa ligi kuu ya England msimu mpya kinatarajia kupulizwa jumapili hii wakati mabingwa Chelsea watakapovaana na Arsenal katika mchezo wa ngao ya jamii.
Mchezo huo utapigwa katika uwanja wa Wembley,London.
Ligi kuu ya Uingereza inatarajia kuanza Agosti 8 kwa michezo sita ambapo Manchester United vs Tottenham katika uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafford wakati Bournemouth vs Aston Villa, Norwich city vs Crystal palace ,Everton vs Watford na Chelsea vs Swansea city.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog
OBAMA ZAWADI ZA KENYA HAKIONDOKA NAZO
Rais Obama hakubeba zawadi yoyote aliyopewa nyumbani kwao Kenya.. Sababu ni hii
Mgeni Rais Obama
alivyoenda kwao Kenya, walijipanga na zawadi kibao ili mtu wao arudi
nazo kwa ajili ya Kumbukumbu Marekani… alienjoy vingi Kenya ikiwemo
dance ya nguvu na wakali wa Sauti Sol, lakini kumbe zile zawadi hata hakuondoka nazo !!
Hata usiwaze kwamba labda Barack Obama
alidharau zawadi ya Kinyago cha Tembo pamoja na picha mbili za kuchorwa
kwa mkono, ishu ni kwamba itifaki au protocol ya Ikulu ya Marekani
hairuhusu Rais wao kupokea zawadi yoyote toka kwa Kiongozi yoyote nje ya
Marekani !
Hizi ndio pichaz za zawadi zenyewe alizopewa Rais Obama toka kwa Rais Kenyatta.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog
UZI WA STAND UNITED HUU HAPA
Aina ya jezi za kisasa watakazotumia Stand United msimu ujao picha zipo hapa
Ligi Kuu soka Tanzania bara kwa miaka kadhaa nyuma kabla ya kuzaliwa kwa klabu ya Azam FC ilikuwa ni ligi ambayo ina ushindani wa kweli kwa timu mbili pekee Simba na Yanga ndizo zilizokuwa na uwezo wa kutwaa taji la Ligi Kuu kwa kupokezana kama sio timu moja wapo kutwaa mara mbili mfululizo.
Hali hii haikutokana kwa sababu ya
ukubwa wa vilabu, hali hii haikutokana kwa sababu ya kuwa na mashabiki
wengi ila ukweli ni vilabu vingi vilikuwa vikikumbwa na tatizo la
kifedha mfano msimu mmoja nyuma tuliwahi kusikia maisha na mazingira
mabovu waliokuwa wanaishi wachezaji wa Stand United kitu ambacho kingeweza kuwa kigumu kuleta ushindani kwa Yanga, Simba na Azam FC.
Baada ya kampuni ya ACACIA inayojishughulisha na masuala ya uchimbaji wa madini kuidhamini klabu ya Stand United, yameanza kutokea mabadiliko chanya kiasi kwamba msimu ujao inawezekana Stand United ikafanya vizuri. Baada ya kumleta kocha wa kifaransa Patrick Liewig kuinoa klabu yao, July 30 imeonyesha aina ya jezi za kisasa itakazotumia msimu ujao.
ACACIA ni kampuni inayomiliki migodi mitatu ya uchimbaji dhahabu Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara, imeingia mkataba wa udhamini na Stand United katika kipindi cha miaka miwili.
SOMA HABARI KUBWA ZILIZOPEWA UZITO MAGAZETI YA LEO, JULY 31TZ
Uchambuzi huu wa magazeti unaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha Candle Euducation Centre Tanga, kituo kinaongoza kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sita na wanaojiendeleza kielimu. Kituo kinatoa kozi mbalimbali za kitaaluma na kielimu. Wapo Tanga mkabala na Bank ya CRDB simu 0715 772746
MWANANCHI
Wabunge wawili waliohama CCM hivi karibuni, James Lembeli na Ester Bulaya wamepitishwa katika kura za maoni kuwania ubunge kupitia chama chao kipya.
Wakati Lembeli akipitishwa kwa kura za kishindo kuwania ubunge katika Jimbo la Kahama Mjini, Bulaya alishinda katika nafasi ya viti maalumu baada ya kushindwa katika kinyang’anyiro cha Jimbo la Bunda Mjini.
Wanasiasa hao sasa wanasubiri uteuzi wa Kamati Kuu ya Chadema utakaofanyika Agosti 5 na 6.
Katika uchaguzi huo wa juzi, mbunge huyo wa zamani wa Kahama aliwabwaga wenzake 13 aliogombea nao akipata kura 168 kati ya 262 zilizopigwa, akifuatiwa na John Katibu aliyepata kura 45, Peter Shita (17) na Emmanuel Madoshi aliyepata kura 10.
Wengine ni Muta Nyerere (4), Felician Maige (4), Zacharia Obadia (3), Tadeo Mwati (2), Arnold Mtajwaka (2), Prosper Denga (2), Deusdedit Madinda (1), Reuben Macheyeki (1). Victor Mbwana na Richard Makingi waliambulia patupu. Katika uchaguzi wa viti maalumu, Winfrida Mwinula alishinda kwa kura 34 akifuatiwa na Salome Makamba aliyepata kura 30.
Kama isingekuwa ni kura za maoni za viti maalumu zilizomfuta machozi, Bulaya alikuwa tayari ametupwa nje baada ya kuanguka katika Jimbo la Bunda Mjini.
Bulaya aliyekuwa miongoni mwa makada saba wa chama hicho waliokuwa wanawania kuliwakilisha jimbo hilo, alipata kura 37 kati ya 182 zilizopigwa akiwa nyuma ya Pius Masururi aliyeibuka mshindi kwa kura 65 na Magembe Makoye aliyepata kura 40.
Baadaye katika mkutano wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha), uliofanyika baadaye usiku, Bulaya alipata kura 71 kati ya 110 zilizopigwa na kuwabwaga Godliver Masamaki aliyepata kura 31, Joyce Sokombi (4), Minza Shani (3), Dk Jane Nyamsenda (1) na Alice Wandya aliyeambulia patupu.
Awali, Bulaya alikwaa kisiki baada ya jina lake kuwa miongoni mwa waliokatwa na kamati ya utendaji inayosimamia majimbo hayo wakidaiwa ni wageni katika chama; wapenda fujo na matabaka, akiwa pamoja na Chacha Nyamhanga, Sulemani Daudi lakini walirudishwa kundini baada ya kikao cha viongozi na watiania.
Katika Jimbo la Bunda Vijijini, Sulemani Daudi aliibuka mshindi kwa kura 84 kati ya 127 zilizopigwana kuwashinda John Masenza aliyepata kura 14, Dk Lucas Webiro (11), Frank Mongateko (8), Edgar Chibura (5) na Mathias Bandio aliyepata kura mo
MWANANCHI
Tume ya Uchaguzi (NEC) leo imetangaza kuongeza siku nne zaidi za uandikishaji wa wapigakura kwa kutumia teknolojia ya BVR baada ya idadi kubwa ya wakazi wa Dar es Salaam kuitikia wito wa zoezi hilo.
Awali zoezi hilo lilikuwa likamilike kesho, Julai 31, lakini sasa litaendelea hadi Agosti 4, mwaka huu ili kukabiliana na idadi kubwa ya watu waliojitokeza kujiandikisha.
Kwa mujibu wa chombo hicho chenye mamlaka ya kusimamia shughuli zote za uchaguzi nchini, hadi jana, zaidi ya wakazi 1,000,000 walikuwa wamekwishaandikishwa jijini Dar es Salaam.
Ikizingatia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, Nec inatarajia kuandikisha jumla ya wakazi zaidi ya 2.8 milioni wa jiji hilo lenye idadi kubwa ya watu nchini Tanzania.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian Lubuva, hadi sasa jumla ya zaidi ya watu 18 milioni wamekwishajiandikisha wakati tume ilitarajia kuandikisha watu kati ya 22 milioni na 23 milioni.
NIPASHE
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), inatarajia kuanza kuwasaka viongozi wa umma waliotumia nafasi zao vibaya ikiwamo kuiba na kujilimbikizia mali ndani na nje ya nchi.
Viongozi hao watasakwa na Takukuru kupitia kitengo maalum kilichoanzishwa mwaka jana ambacho kimeanza kupewa mafunzo nchini Uingereza.
Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk. Edward Hoseah (pichani), aliyasema hayo jijini Dar es Salaam juzi alipokuwa akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari.
Dk. Hoseah aliyasema hayo muda mfupi baada ya kufungua mafunzo ya watumishi wa Takukuru ambao wapo katika kitengo hicho ili kuwajengea mbinu na uwezo wa kufanya uchunguzi dhidi ya viongozi walioiba na kujilimbikizia mali.
Alisema kitengo hicho cha Takukuru pia kitakuwa na kazi ya kupambana na masuala ya utakatishaji wa fedha haramu kwa kuwa tatizo hilo linazidi kukua hapa nchini.
Aliongeza kuwa kitengo hicho kilianzishwa rasmi mwaka jana, lakini hakikuanza kazi yake kutokana na kuchelewa kupatikana mtalaam wa kutoa mafunzo kwa watumishi hao.
”Tumejizatiti kukabiliana na viongozi wa umma waliojilimbikizia mali kwa kutumia watalaam wetu ambao wanapatiwa mafunzo,” alisema.
Dk. Hoseah alisema huu ni mwanzo na kwamba watahakikisha wanafanya kazi vizuri ili kuwabaini watu walioiba na kujilimbilikizia mali huku akisema kwamba sheria ni msemeno
Kuhusu wanasiasa wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa hususan katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu, Dk. Hoseah alisema mtu yeyote asithubutu kufanya hivyo kwa kuwa Takukuru imesambaa kila wilaya na kwamba watakamatwa.
”Hawa wagombea wasifanye mchezo mchafu, ninawaonya kwa kuwa tutawakamata popote walipo,” alisisitiza.
Aliwaonya wanasiasa wanapita maeneo mbalimbali na kuanza kuchonga barabara na kutoa zawadi nyingine kwa kuwa kufanya hivyo ni kosa na Takukuru itawashughulikia.
Aliongeza kuwa mtu yeyote atakayepindisha sheria kwamba Takukuru ipo macho muda wote na itawamulika wanasiasa ama wapambe wao ambao watataka kuwahonga wananchi kuwashawishi wawapigie kura.
Hata hivyo, kauli ya Dk. Hoseah imekuwa ya kawaida kutolewa kwa kuwa aliwahi kutangaza vita na wala rushwa wakubwa hapa nchini huku akiahidi kuwaburuza mahakamani, lakini mpaka leo hakufanya hivyo.
NIPASHE
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, amekanusha kumshushia kipigo Dk. Joseph Chilongani, ambaye ni mgombea mwenzake katika mchakato wa Chama Cha mapinduzi (CCM), kupata mgombea ubunge Jimbo la Kongwa.
Awali ilidaiwa kuwa Jumatatu jioni Ndugai, alitumia fimbo kumpiga Dk. Chilongani, ambaye alipoteza fahamu kabla ya kupelekwa hospitali ya wilaya hiyo, ambako aliendelea na matibabu mpaka jana aliporuhusiwa.
Mganga Mkuu wa Wilaya, Festo Mapunda, alilieleza NIPASHE jana kuwa walimruhusu kutokana na hali yake kiafya kuwa nzuri.
Naye Naibu Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, hakuwa tayari kueleza ikiwa mpaka jana alikuwa amepokea taarifa rasmi ya tukio hilo kutoka kwa walalamikaji badala yake alisema Dk. Chilongani, jana aliendelea na kufanya kampeni kama kawaida.
Madai dhidi ya Ndugai yalielezwa na Dk. Chilongani, kuwa sababu ya mtafaruku huo ilikuwa mzozo uliyoibuka kati ya Ndugai na mgombea mwingine, Simon Ngatunga, na baadaye Ndugai kumtuhumu Dk.
Chilongani kuwa alikuwa akitumia simu yake ya kiganjani, kumrekodi video ili kusambaza mitandaoni. Hata hivyo Ndugai alisema jana kuwa miongoni mwa wagombea tisa wanaowania nafasi hiyo, baadhi wamepandikizwa kwa lengo la kufanyia fujo.
“Tangu tuanze kampeni, wagombea mapandikizi wanafanya kazi ya kunitukana na kunidhalilisha kila tunakokwenda, mmoja ananiporomoshea matuzi ikitokea nikajibu, wanakuwa wameshapanga mmoja wao wa kunirekodi ili wazidi kunidhalilisha mitandaoni,” alieleza Ndugai
Alisema tukio la Jumatatu, wakiwa kwenye mkutano wa hadhara Ngatunga, alimtukana matusi ya nguoni na kusababisha mzozo kati yao, wakati watu wakiendelea kumsihi ampuuze yule kijana huyo akagundua Dk. Chilongani akitumia simu yake kumrekodi.
“Nilishamuonya mara kadhaa aache kujifanya mwandishi wa habari, kwa kuachukua video tena akinilenga mimi tu, lakini hakusikia nilichofanya niliigonga ile simu aliyokuwa akiitumia kuchukua video,” Ndugai alisema.
“Nikaigonga nikimwambia hebu usiendelee kunichukua video na kikamera chako hicho simu ikaanguka chini, nikashangaa kuona na yeye akijiangusha chini kama wachezaji wa mpira wa miguu, ambao hujiangusha kwa lengo la kusingizia wamefanyiwa fujo ili wenzao wapewe kadi nyekundu.”
Kwa mujibu wa Ndugai, hakumpiga Dk. Chilongani wala hakujaribu kumpiga Ngatunga.
NIPASHE
Hofu imetanda ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na wananchi kwa ujumla kutokana na kutoonekana kwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, katika matukio mawili makubwa ya kisiasa yanayohusu mustakabali wa chama hicho.
Dk. Slaa hakuonekana siku ya kihistoria Jumanne wiki hii, iliyokuwa maalum kwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, kutangaza kujivua uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga Chadema.
Kadhalika, Dk. Slaa hakuonekana jana makao makuu ya chama wakati Lowassa alipofika kuchukua fomu ya kuwania urais kupitia chama hicho akitarajiwa kuwakilisha Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi (Ukawa), katika hafla iliyotikisa jiji la Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi wa juu wa Chadema.
Hata hivyo, Dk. Slaa alihudhuria kikao cha dharura cha kamati kuu ya Chadema Jumapili iliyopita ambacho kiliendelea hadi usiku wa manene na hoja kuu ikiwa ni kujadiliana na Lowassa na kumpokea katika chama hicho.
Dk. Slaa alionekana katika baadhi ya picha zilizovuja kutoka katika kikao hicho akiwa na viongozi waandamizi wa Chadema huku akijadili jambo na Lowassa, ambaye katika siku za hivi karibuni ambekuwa gumzo kubwa baada ya kubadili upepo wa siasa za Tanzania.
Tangu juzi kumekuwa na mijadala mirefu ndani ya mitandao ya kijamii, juu ya aliko Dk. Slaa, wengine wakibashiri kuwa ameamua kuacha siasa.
Hata hivyo, Dk. Slaa mwenyewe hajawa radhi ama kupokea simu yake au kujitokeza hadharani kujibu maswali ya umma juu ya kinachomsibu.
Mbali na kutokuonekana Chadema, Dk. Slaa pia hakuonekana kwenye mkutano wa Ukawa, uliofanyika Jumatatu wiki hii makao makuu ya Chama cha Wananchi (CUF), ambao wenyeviti wenza wa umoja huo walimkaribisha Lowassa kujiunga nao.
Wakati wa Dk. Slaa akiadimika kwenye hadhara, viongozi waandamizi wa Chadema kwa nyakati tofauti wameithibitishia NIPASHE kuwa kila kitu “kimedhibitiwa” kuhusu tetesi kwamba kiongozi huyo amesusa.
“Sikiliza brother Dokta yuko freshi. Kila kitu kinakwenda kama tulivyopanga. Hakuna ukweli wa lolote juu ya madai eti Dokta anakwenda CCM,” kilisema chanzo chetu kilichoomba kutotajwa kwa sasa.
Wakati hali ikiwa hivyo, kuna taarifa kwamba Dk. Slaa anashinikizwa sana na watu wa ndani ya familia yake ambao wanadaiwa kusumbuliwa zaidi na ubinafsi, hasa baada ya mabadiliko ya kisiasa ambayo yamekikumba chama hicho kufuatia kujiunga kwa Lowassa.
Watu hao wa ndani wa familia ya Dk. Slaa wanadaiwa kuwa walikuwa wamejiandaa kuwa sehemu ya harakati za katibu mkuu huyo kuwania tena urais mwaka huu kama ilivyokuwa mwaka 2010.
“Sisi tunawaza jinsi ya kuivunjavunja CCM, lakini wapo watu wanawaza jinsi ya kuwa sijui nini sijui nani?
Hapa tunatafuta njia ya kuing’oa CCM hata kama ni kwa kutumia nguvu ya shetani,” alisema kiongozi mmoja wa Chadema.
Lowassa aliamua kujiunga Chadema baada ya kuchoshwa na siasa zilizojaa chuki za kumzuia kuingia kwenye kinyang’anyiro cha kusaka tiketi ya kuwania urais kupitia CCM.
Katika hatua nyingine, Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu, aliliambia NIPASHE kwamba, Dk. Slaa alishiriki vikao vyote muhimu vilivyoafiki, Lowassa kujiunga na chama hicho.
“Jana (juzi) usiku nilikuwa naye na wiki hii alishirika kikao cha kamati kuu ambacho mliona picha kwenye mitandao,” alisema.
Alipoulizwa alipo, Dk. Slaa, Lissu hakutoa majibu ya moja kwa moja zaidi ya kusema kwamba akiwapo mwenyekiti kwenye kikao chochote inatosha na siyo lazima, viongozi wote wa kitaifa wawepo.
Kuhusu Naibu Katibu wa Chadema, Tanzania Bara, John Mnyika na yeye kutoonekana katika mikutano hiyo, alijibu kwa kifupi kwamba anaumwa.
Licha ya kutafutwa mara kadhaa kupitia simu yake ya mkononi juzi na jana, Dk. Slaa hakupatikana badala yake mtu mmoja mwanamke alipokea na kusema mpigaji amekosea namba.
Alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno ili aeleze kilichomsibu kushindwa kuhudhuria matukio muhimu ya kumkaribisha Lowassa pia hakujibu.
NIPASHE
Mgombea wa urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli (pichani), ameiomba serikali kuendelea kujenga barabara ya lami awamu ya pili hadi makao makuu ya Wilaya ya Simanjiro toka KIA, huku akiwataka Watanzania kukataa watu wanaowatenganisha kwa misingi ya ukabili, dini na vyama vya siasa.
Alitoa wito huo jana wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya lami ya kilomita 26 toka KIA hadi Mererani, Manyara iliyohudhuriwa na Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Bilal.
Alisema ni vizuri Watanzania wakaendeleza na kuwaogopa baadhi ya watu wanaotaka kuwatenganisha kwa misingi ya vyama, ukabila na udini, kwani hakuna tija kwa Taifa.
“Haya maendeleo hayachagui ukabila, dini wala vyama vya siasa, ndio sababu serikali inajenga barabara kila mahali bila kujali chama gani kipo mahali hapo, hiyo ndiyo misingi tulionayo,” alisema.
Alimuomba Makamu wa Rais kuendeleza barabara hiyo hadi makao makuu ya Simanjiro, katika awamu ya pili baada ya kumalizika awamu ya kwanza.
Dk. Magufuli alisema ujenzi wa barabara ya KIA hadi Mererani amekabidhiwa mkandarasi China Hennan International Cooperation Group Co. Ltd , ambaye alimtaka kuikamilisha kwa wakati.
Alisema ujenzi wa barabara hiyo utagharimu Sh. bilioni 32.2 na kumtaka mkandarasi huyo kuajiri vijana wa eneo hilo ili nao wanufaike na matunda ya miradi ya eneo lao.
Alisema hadi sasa serikali inaendelea na ujenzi wa barabara za lami kilomita. zaidi ya 17,000 kati ya hizo 5,500 zimekamilika kwa kiwango cha lami, jambo ambalo ni la kupongezwa na kila mpenda maendeleo.
Alisema barabara hiyo ina umuhimu mkubwa kutokana na kuwapo kwa machimbo ya madini ya Tanzanite ambayo yanaingizia mapato makubwa serikalini.
Dk. Bilal alimsifia Dk. Magufuli kuwa ni jembe na anastahili kupeperusha bendera ya urais ya CCM, kutokana na kazi alizofanya bila kutetereka.
Aliwaomba wananchi kuacha kuhujumu mradi huo kwa kuiba vifaa, badala yake wavilinde ili kumpa moyo mkandarasi.
“Lakini nimepokea ombi la Dk. Magufuli la kutaka barabara iendelee awamu ya pili hadi makao makuu ya wilaya na itakuwa hivyo, pia tutafikiria kuyaleta maji eneo hili haraka iwezekanavyo,” alisema.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale, alisema barabara hiyo itakuwa na vituo vya mabasi vitano na madaraja matano na inakadiriwa kudumu kwa miaka 20.’
MTANZANIA
Idara ya uhamiaji nchini imesema inawashikilia wahamiaji haramu 2,048 kutoka nchi mbalimbali kwa tuhuma za kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura.
Naibu kamishna wa uhamiaji na msemaji mkuu wa idara hiyo, Abbas Mussa alisema jana kuwa wahamiaji hao wanatoka nchi za Kenya, Burundi na Uganda.
Alisema walikamatwa katika mikoa 14 wakijifanya ni Watanzania, lakini ilibainika kuwa siyo raia baada ya idara hiyo kufanya uchunguzi kwenye vituo vya uandikishaji.
“Baadhi yao tumewafikisha mahakamani, lakini wengine bado uchunguzi unaendelea na wakibainika nao watachukuliwa hatua,” alisema Mussa.
Aliongeza kuwa wengi ya wahamiaji hao walifika mikoa ya Kagera, Mara, Tanga, Kigoma, Rukwa, Kilimanjaro, Ruvuma, Geita, Shinyanga, Mtwara, Pwani, Mbeya, Morogoro na Dar es Salaam.
“Inasikitisha sana, kwani baadhi ya waliokamatwa walishajiandikisha na kupewa vitambulisho kama raia wa Tanzania,” alisema.
Alisema kutokana na hali hiyo, Idara imeamua kuongeza maofisa katika vituo ili kuendelea kuwabaini wahamiaji hao.
Mussa aliwataka wananchi kutoa taarifa mara wanapobaini watu ambao siyo raia wanajiandikisha.
Aliongeza kuwa maombi ya hati za kusafiria yameongezeka maradufu kutoka hati 4,938 Julai 2014 hadi 8,703 Julai 2015 kwa upande wa Bara na kutoka hati 588 Julai 2014 hadi hati 1,028 Juni 2015 kwa upande wa Zanzibar.
Alisema idara inawataarifu wananchi kuwa siyo lazima kubadilisha hati inapokwisha muda wake, badala yake mmiliki anaweza kubadili na kupatiwa nyingine wakati wowote atakapokuwa akisafiri.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog
Thursday, July 30, 2015
WANAOFANYA MGOMO WA KULA GEREANI ISRAEL , KUKIONA
Sheria mpya kwa wafungwa kulishwa chakula wakileta mgomo…
Sheria hiyo ambayo ilikubaliwa na idadi
kubwa ya wabunge, inawaruhusu mahakimu kuhakikisha kuwa wafungwa
wanalishwa kwa lazima na pia kupata matibabu kwa lazima bila ya ruhusa
ya mfungwa ili kunusuru maisha yao.
Raia wa Palestina ambao wanazuiliwa
katika magereza ya Israeli wamekuwa wakisusia chakula kama njia yao ya
kupinga kukamatwa kwao katika miaka michache iliyopita.
Nchi hiyo inahofu kuwa wafungwa hao ambao wamekataa kula chakula huenda wakafa na kusababisha fujo magerezani.
Sheria hiyo mpya imelaaniwa na chama cha
madaktari nchini Israeli, ambacho kinaamini kuwa kuwalisha wafungwa
chakula kwa nguvu ni mbinu ya mateso na ni hatari kimatibabu.
Kwa habari,matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog
VIMBWANGA VYA WALIMWENGU
Stori ya mwanamke kuripotiwa kufa na baadaye kukutwa hai isikupite mtu wangu…
Kuna stori moja iliwahi kuripotiwa Bagamoyo baada ya maiti kuzua taharuki kwa waombolezaji wakidai hajafa licha ya kudhibitishwa na daktari kuwa alifariki.
Huko Ujerumani mwanamke mmoja anayekadiriwa kuwa na miaka 92 ambaye aliaminika kupoteza maisha kisha mwili wake kuhifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti amezua gumzo.
Tayari daktari wa zamu alithibitisha kifo cha mwanamke huyo baada ya kumpima na kuridhika kuwa amefariki ..lakini baada ya masaa machache wahudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti walikuta mwili wa mwanamke huyo ukijigeuza na kugundua alikua hajafariki kama ilivyoripotiwa.
Tukio hilo lilifanya ndugu wa marehemu kushangazwa na hali hiyo huku wakimjia juu daktari aliyewapa taarifa kuwa mgonjwa wao amefariki duniani na kutaka walipwe fidia.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog
FACE BOOK KIDEDEA
Facebook Vs Instagram nani ana watumiaji wengi zaidi duniani? Majibu yake haya hapa.
Kama wewe ni miongoni mwa wale watu wanaohisi Facebook ni mtandao uliopitwa na wakati, basi utapenda kusikia taarifa hii.
Mwishoni mwa mwezi wa sita kampuni ya FB Tech30 ama Facebook ilitajwa kuwa na watumiaji takribani bilion 1.5 kwa mwezi tu, watu wanaoutumia mtandao wa Facebook duniani kwa mwezi tu unazidi matumizi ya mitandao mengine duniani kama Microsoft (MSFT Tech30).
Ukuaji wa namna hii umeiruhusu Facebook kubuni features tofauti ili kuwezesha kampuni hiyo kukusanya data na taarifa tofauti za watumiaji wa mtandao huo.
Licha ya hayo ofa ya matangazo yanyotolewa na Facebook imewaingizia kampuni hiyo zaidi ya dola Bil 3.8 ambalo ni ongezeko la 43% ya ukuaji wao toka mwaka jana…Ofa ya matangazo ya facebook kupitia simu za mkononi inawaingizia zaidi ya dola Bil 2.9 na zaidi ya 62% ya mapato ndani ya miaka 3.
Facebook imeendelea kukua na kwa sasa imeweza kuwapiga gepu washindani wake wakubwa kama Twitter (TWTR, Tech30). Jumanne ya wiki hii Interim CEO wa Twitter Jack Dorsey alisema kuwa ukuaji wa Twitter umekuwa ukishuka kwasababu watu wengi hawaelewi kwanini wanahitaji kuutumia mtandao huo.
Mwanzilishi na Mkurugenzi wa mtandao wa Facebook, Mark Zuckerberg
amesema kuwa mafanikio makubwa ya mtandao huo ni dhamiria rahisi ya
kuelewa namna ya kurahisisha mawasiliano na wanajitahidi kukuza na
kusupport vitu vinavyo ibeba dhamira hiyo.
Licha ya Instagram
kuwa maarufu sana kwa matumizi ya watu wengi siku hizi idadi ya
watumiaji wa mtandao huo ni 26% duniani wakati idadi ya watumiaji wa Facebook duniani ni 71% na kwa zaidi ya miaka 3 iliopita wamekuwa product ya teknolojia inayotumiwa zaidi duniani.
Kwa habai, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog
CHEMCHEM ILIYOSAHAULIKA KIJIJI CHA MAJIMOTO AMBONI ,TANGA
Tangakumekuchablog
Tanga, WAKAZI
wa kijiji cha Majimoto kata ya Mafuriko halmashauri ya jiji la Tanga,
wameshangazwa na Wizara ya Utalii na Maliasili kuacha kuifanya chemchem inayotoa maji moto iliyoko kijiji hapo kuwa ya kitalii hatua ambayo inaikosesha Serikali mapato.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti
jana, wakazi hao walisema Chemchem hiyo imekuwa kivutio jambo ambalo wageni
kutoka mataifa ya nje hufika na kujionea maajabu ilhali Serikali imeshindwa
kuitambua.
Alisema kutokana na kutokuwepo kwa
utaratibu wageni wa nje na ndani hufika bila kizuizi na kujionea maajabu ya
Chemchem hiyo ambayo hutoa maji ya moto pamoja na maajabu mengine yaliyopo eneo
hilo.
“Serikali inatambua uwepo wa
chemchem hii inayotoa maji moto si usiku wala mchana na haina kiangazi wala
masika----raia wa kigeni wanaitambua ila sisi hatuna habari nayo” alisema Hamad
Pinto na kuongeza
“Kama Serikali ingeweka utaratibu wa
kukiweka kituo hiki katika mazingira ya utalii ingeweza kuongeza mapato
yake-----watu wanakuja bila mpangilio na
kupiga picha na kushangaa shangaa” alisema
Kwa upande wake mkazi wa Amboni,
Mussa Juma, alisema kuna vivutio vingi vya utalii eneo hilo lakini
havitambuliki yakiwemo majengo ya kale na misitu yenye wanyama.
Alisema kama Serikali
ingeliviendeleza vivutio hivyo na vijana kupata ajira na kuondokana na ukaaji wa
vijiweni jambo ambalo linawasukuma kujitumbukiza katika viwashawishi.
Alisema vijana wengi hawana kazi na
wamekuwa wakikaa vijiweni hivyo kuwepo kwa vivutio hivyo na kuendelezwa ingweza
kupunguza wimbi la umasikini na ajira kwa vijana.
“Vinaja wengi hawana ajira wala kazi
ya kujiajiri na badala yake wamekuwa wakikaa vijiweni kupiga soga-----kama
vivutio vya kitalii vipo kuna sababu gani ya kuacha kuendelezwa” alisema Juma
Alisema ili kuweza kupunguza
umasikini ni vyema Serikali kuviendeleza vivutio vyake jambo ambalo linaweza kuingiza
mapato na kuweza kupunguza umasikini majumbani.
MARADONA VITUKO HADI MITAANI
Vituko vya Maradona haviishi!! safari hii kamtuhumu mke wake kumwibia fedha
Mkongwe wa soka duniani Diego Maradona amerudi kwenye headlines tena baada ya kumtuhumu mke wake wa zamani Claudia Villafane kuwa amemuibia fedha kwenye akaunti yake.
Maradona akizungumza kwenye matangazo ya moja kwa moja ya Televisheni alisema Villafañe ambaye alikuwa mpenzi wake wa zamani ni mwizi na amemwibia kiasi cha dola milioni 9 benki.
Hata hivyo Villafañe amepinga vikali
madai hayo na kudai kuwa yeye si mwizi na hakuiba fedha hizo huku
akitetewa pia na watoto wake Dalma na Giannina kwenye mtandao wa twitter.
Wapenzi hao ambao walikutana miaka ya zamani katika mji uliokithiri kwa umasikini huko Buenos Aires kabla
ya Maradonna kuwa maarufu na kuwa miongoni mwa wachezaji mahiri duniani
katika historia ya soka,waliachana baada ya kutofautiana.
Watoto wao wawili Dalma and Giannina,wamekaririwa kwenye mtandao wa twitter wakimtetea mama yao wazi wazi na kwamba hahusiki na upotevu huo wa fedha za baba yao.Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog
SOMA KURASA MWANZO MWISHO YA MAGAZETI YA LEO, JULY 30 TZ
Magazeti yanaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha Candle Education Centre Tanga, kituo kinaongoza kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sita na wanaojiendeleza kielimu, Kituo kinatoa kozi mbalimbali za kielimu na kitaalamu zikiwemo za Ufundi wa Computer. Kituo kipo Tanga mkabala na Bank ya CRDB simu 0715 772746
Subscribe to:
Posts (Atom)