Sunday, July 12, 2015

GWIJI LA UCHEKESHAJI AFRIKA MASHARIKI AFARIKI

MZEE OJWANG WA VITIMBI AFARIKI DUNIA JIJINI NAIROBI

ojwang
Mwigizaji maarufu kutoka nchini Kenya  Mzee Ojwang amefaiki jana jumapili jioni katika hospitali ya  Kenyatta jijini Nairobi alikokuwa amelazwa , Mwigizaji  Benson Wanjau alisema  Mzee Ojwang .  alikuwa amelazwa hospitalini hapo akisumbuliwa na  ugonjwa wa Pneumonia. Ojwang alikuwa mwigizaji wa vipindi maarufu vya  Vitimbi, Vioja Mahakami, Vituko na Kinyonga katika vituo vya luninga vya Kenya na ITV nchini Tanzania
Alijipatia umaarufu nchini Kenya pamoja na maeneo yote ya nchi za Afrika Mashariki kutokana na uwezo wake katika kuigiza ambapo alikuwa akiwavunja mbavu watazamaji wake kutokana na vituko vyake na uwezo wake katika kuchekesha watazamaji wakati akiigiza.
Tanga kumekucha itakusogezea kila kinachojiri ndani na nje ya nchi, ni hapa hapa 

No comments:

Post a Comment