Monday, July 13, 2015

BANK YA DTB YAFUTARISHA TANGA



Tangakumekuchablog
Tanga, MSTAHIKI Meya halmashauri ya jiji la Tanga, Omary Guledi, ameitaka jamii kushikamana na kuvumiliana kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu ili kuliwezesha Taifa kuvuka  kwa amani kipindi cha kampeni na uchaguzi.
Akizungumza wakati futari iliyoandaliwa na Bank ya Diamond  Trust  Bank (DTB) kwa kushirikiana na mshirika wake, Express Global Money, Guledi alisema kipindi hiki kuelekea uchaguzi jamii inatakiwa kuvumiliana na kuitunza amani iliyopo.
Aliitaka jamii kuacha kushabikia vyama vya siasa hadi kupelekea  kuhasimiana na hivyo kuitaka kupima sera  za wagombea   viongozi wenye uwezo wa kuongoza na wanaoweza kusukuma mbele  maendeleo.
“Kupitia hadhara hii ni fursa adhimu kutoa ujumbe kwa wananchi hasa kipindi hiki tunachoelekea uchaguzi mkuu----kitu cha msingi zaidi ni suala la amani na utulivu uliopo” alisema Guledi na kuongeza
“Tuwasikilize wanasiasa wanavyojinadi na kutoa sera zao ila tuwe makini siku ya kuchagua----tusichague kwa kuangalia sura wala nasaba kinachotakiwa ni uadilifu na kiu ya maendeleo” alisema
Aliwataka wananchi kuwapima wagombea wanaotaka kura zao kwa sera na vipaumbele vyao na kuepuka kuchagua wagombea kwa kuangalia sura na nasaba jambo ambalo linaweza kuwaongezea umasikini majumbani.
Kwa upande wake mkuu wa kitengo cha masoko Bank ya (DTB) , Sivlester  Bahati, alisema bank hiyo imeviwezesha vikundi mbalimbali vya ujasiriamali wanawake kuwapa mikopo na  kutoa mbinu za kuwa wajasiriamali wakubwa .
Alisema bank hiyo iko na mikakati ya kumuenua mwananchi wa kipato cha chini kuwekeza kwa kuweka akiba kadri ya uwezo wake na kufaidika fursa ya mikopo na bank kumpa mbinu za kuanzisha mradi ambao atamuwezesha kurejesha rejesho..
“Bank yetu iko na mipango kemukemu ya kumuenua mwananchi wa kipato cha chini----tunampa elimu ya ujasiriamali na mbinu ya kuwekeza kasha kukopa na kurejesha” alisema Bahati
Alisema bank hiyo iko na mikakati ya kufungua matawi kila Wilaya lengo likiwa ni kumfikia mwananchi wa hali ya chini pamoja na wafanyabiashara ili kuepuka wizi na uporaji .
                                                     Mwisho


 Waumini wa dini ya Kiislamu na wakazi wa Tanga wakishiriki katika futari iliyoandaliwa na Bank ya Diamond Trust Bank (DTB) kwa kushirikiana na mshirika wao, Express Global Money  juzi, ambapo zaidi ya watu 300 walishiriki na kuongozwa na Meya wa jiji la Tanga, Omary Guledi.

No comments:

Post a Comment