Friday, July 10, 2015

NILIJUA NIMEUA SEHEMU YA (3)

HADITHI hii inaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Tiba Asilia Cha Mkombozi Sanitarium Clinic. Mabingwa wa magonjwa sugu na yaliyoshindikana. Mkombozi wa ko na mashine za kisasa za kupima mwili mzima kwa gharama nafuu. Wapo Tanga eneo la Chuda mkabala na Rahaleo. simu 0654 361333
 
NILIJUA NIMEUA 3
 
ILIPOISHIA
 
Aliingia ndani ya teksi akaichukua ile simu na kutoka.
 
“Asante kaka. Kumbe ulikuwa unanitania!”
 
Sote tukacheka. Huzuni ilikuwa imeshamtoka.
 
“Wewe ni muaminifu sana. Nitakuwa nachukua teksi yako kila siku” akaniambia.
 
“Kwaheri, nakwenda zangu” nikamuaga.
 
“Ulikuwa umeniletea simu yangu. Asante sana kaka, endelea kuwa na moyo huo huo”
 
“Asante bibie”
 
Wakati natia gea niondoe gari sauti yake ikanisitisha.
 
“Nipe namba yako. Nitakuhitaji tena siku nyingine”
 
Nikamtajia namba yangu.
 
SASA ENDELEA
 
Akaijaza kwenye simu yake.
 
“Na mimi nipe yako” nikamwambia.
 
“Ngoja nikupigie. Unaitwa nani?”.
 
“Majombi Teksi”
 
Jina hilo likamchekesha. Alipolijaza kwenye simu akanipigia. Simu yangu iliita. Nikaishika na kuitazama.
 
“Hii ndio namba yako”
 
“Ndiyo hiyo”
 
“Unaitwa nani?”
 
“Mariam” akatamka haraka.
 
Nikahifadhi ile namba pamoja na jina lake kwenye simu yangu. Nilipomaliza nikamwambia “Sawa”
 
Nikaiondoa teksi.
 
Huo ukawa mwanzo wa kujuana na Mariam.
 
Kutoka siku ile akawa ananipigia simu mara kwa mara kuniita sehemu kwa ajili ya kuhitaji huduma ya teksi yangu. Kulikuwa na siku ambayo alinipigia simu saa tisa usiku. Nilikuwa nimesharudi nyumbani na nilikuwa nimelala. Nikaamka na kuangalia simu iliyokuwa inaita. Nikaona ni yeye aliyekuwa akinipigia. Nikashituka na kujiuliza kwanini alikuwa ananipigia simu usiku ule, alikuwa wapi na alikuwa na nini?
 
“Hallo Mariam …vipi?” nikamuuliza baada ya kupokea simu yake.
 
Nilikuwa nimekereka kukatishwa usingizi wangu lakini nilivumilia.
 
“Majombi uko wapi?”  Sauti ya Mariam ikauliza.
 
“Niko nyumbani” nikajibu.
 
“Ninakuhitaji hapa Habours Club”
 
Habours ilikuwa klabu ya starehe ambayo ilikuwa ikitumiwa kwa maonesho ya miziki hasa miziki ya taarab.
 
“Unataka nikufuate hapo Habours Club?”  nikamuuliza.
 
“Ndiyo”
 
“Nikupeleke wapi?”
 
“Nyumbani”
 
“Ulikuwa kwenye mziki?”
 
“Ndiyo”
 
Nilisita kumpa jibu. Kwa upende mmoja sikupenda kukatisha usingizi wangu kwani nilihitajika kuamka saa kumi na mbili asubuhi niingie kazini. Kurudi kwangu nyumbani ni saaa sita au saba usiku.
 
Lakini kwa upande mwingine sikutaka kumkatisha tamaa mteja wangu. Kwa vile ilikuwa ni kazi ya usiku nilijua ingeniingizia pesa nzuri. Nikaona nimfuate.
 
“Unasemaje, utanifuata?”  Sauti ya Mariam ikakatisha mawazo yangu.
 
“Mko wangapi?” Nikamuuliza ili kupanga masilahi yangu.
 
“Tuko wawili, mimi na rafiki yangu”
 
“Nisubirini, nakuja”
 
“Sasa ukifika nipigie unishitue kwani tuko ndani”
 
“Sawa, nitakupigia”
 
Mariam akakata simu.
 
Niliondoka kitandani na kuanza kuvaa. Nilikuwa nikiishi eneo la Msambweni kwenye nyumba yangu mwenyewe. Ilikuwa nyumba ya urithi. Tuliirithi mimi na mdogo wangu wa kiume baaada ya baba yetu kufariki dunia.
 
ITAENDELEA KESHO, usiache ukapitwa na uhobdo huu ni kitafuta, ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment