Monday, June 13, 2016

NG'OMBE AKWAMA KWENYE MTI

Kichwa cha ng'ombe chakwama ndani ya mti

Ng'ombe  aliyesakama kichwa chake ndani ya mti mkubwa ameokolewa.
Haijulikani ni vipi ng'ombe huyo aliingiza kichwa chake ndani ya mti huo.
Waokoaji wakishirikiana na wazima moto na daktari wa wanyama walishughulika kumuokoa ng'ombe huyo ambaye kichwa chake kilikuwa ndani ya mti katika kitongoji cha North Yorkshire.
Mmiliki wa ng'ombe huyo aliomba msaada wa dharura Northallerton na shughuli hiyo iliposhindwa kumnusuru ng'ombe wake ikawabidi kuwahusisha wazima moto waliotumia msumemo maalum wa mduara kukata kwa ueledi mti huo bila ya kumjeruhi  na kisha wakamnusuru.
Alikuwa akitupa mateke ilimbidi afisa anayewatibu mifugo kumdunga sindano atulie ili shughuli hiyo ifanikiwe.
.
 Baada ya muda ng'ombe huyo aliokolewa.

No comments:

Post a Comment