Pauni ya Uingereza yazidi kuporomoka
Waziri wa fedha wa Uingereza, bwana George Osborne, amezihakikishia masoko ya Ulaya kuhusu matumaini ya siku zijazo kufuatia kura hiyo ya kujitenga.
Soko la ubadilishanji wa fedha limefunguliwa leo likiwa asilimia 0.8% chini ya kiwango kilichoshuhudiwa ijumaa.
Kigezo cha Soko la hisa la FTSE lilifunguliwa leo likiwa na pointi 6,092.19.
Dhidi ya sarafu ya Ulaya Euro inabadilishwa na €1.2170,ikiwa ni asilimia 1.2% chini ya kiwango cha ijumaa.
Waziri wa fedha bwana Osborne amesema kuwa uchumi wa Uingereza utalazimika kujifunga kibwebwe kwani waingereza watalazimika kusubiri kwa muda kuteuliwa kwa waziri mkuu mpya atakayetoa mwelekeo mwafaka wa taifa.
Huko Asia , serikali zimekuwa zikisaidia soko la ubadilishanaji wa fedha zisiporomoke zaidi na kuathiri vibaya uchumi wa eneo hilo.
BBC
No comments:
Post a Comment