WHO: Pakiti za sigara kukosa maandishi
Kauli hiyo hata hivyo imepingwa vikali na muungano wa kampuni zinazotengeneza sigara duniani ikisema kuwa kamwe kauli hiyo haina msingi wowote.
Kila mwaka takriban watu milioni 6 hufaa kutokana na maambukizi yanayohusishwa na uvutaji sigara.
Upakiaji wa sigara katika mapakiti yasiyokuwa na maandishi yeyote ila yale ya kutahadhari watu dhidi ya uvutaji sigara yamepigiwa upatu kupunguza hamu ya kuwavutia wateja wapya wa kuvuta sigara.
Kulingana na mpango huo wa WHO mapakiti hayo yatakuwa na nembo zisizovutia na zenye rangi moja.
Tangu Australia ilipoweka sheria hii mwaka wa 2012 uvutaji sigara ulipungua kwa asili mia 0.55% ambayo ni sawa na takriban watu 108,000 kati ya mwezi Desemba 2012 na Septemba 2015 taarifa hiyo ya WHO inaelezea.
BBC
No comments:
Post a Comment