Monday, April 11, 2016

KINGWANGALWA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA BOMBO TANGA

  Naibu Waziri wa Afya, Hamis Kigwangala, akisalimiana na watoto walipolazwa katika wodi ya watoto hospitali ya Mkoa ya Bombo Tanga wakati alipofanya ziara yake hospitalini hapo leo.


Tangakumekuchablog
Tanga, NAIBU Waziri wa Afya, Hamis Kigwangala, amewataka Madaktari na Wakuu wa Idara katika hospitali nchini kufanya kazi kwa bidii na kusema kuwa Serikali inataka kutumia           mfumo wa Elekronic na kuondokana na makaratasi.
Akizungmza na madaktari na wafanyakazi wa hospitali ya Bomb oleo wakati wa ziara yake ya kujionea utendaji kazi na changamoto zinazowakabili, Kigwangala amesema Serikali ya awahi ya tano haitaki wafanyakazi wazembe.
Amesema kila mtumishi anapaswa kufanya kazi kwa weledi ili kuondosha manung’uniko ya wananchi hivyo kuwataka kujituma.
Amesema Serikali inataka kuondosha mfumo wa kuweka kumbukumbu katika makaratasi na badala yake kuweka kwa mfumo wa Elektoroniki  ili kuweza kufanya kazi kwa wepesi na weledi.
Naibu huyo amefurahishwa na mazingira ya hospitali hiyo na kusema kuwa jitihada zinatakiwa kuongezwa ikiwa na pamoja na kuwahudumia wagonjwa.
                                          Mwisho






 Naibu Waziri wa Afya, Hamis Kigwangala, akishuka ngazi kutoka wodi ya watoto hospitali ya Bombo wakati alipofanya ziara yake leo.





 Katibu wa Afya hospitali ya Bombo Tanga, Adam Katundu, akitaka ufafanuzi wa jambo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Afya, Hamis Kigwangala wakati alipofanya ziara hospitalini hapo leo.
Daktari hospitali ya Safi Medics ya Tanga, Joseph Mbaresero, akiuliza swali kwa Naibu Waziri wa Afya, Hamis Kigwangala, wakati alipofanya ziara  hospitali ya Bombo  leo.

No comments:

Post a Comment