Ndege isiyotumia mafuta yatua Misri
Haikutumia mafuta ya ndege ya kawaida hata chembe bali nguvu za kawi zinazotokana na miali ya jua.
Marubani wawili wa Uswizi ndio wanaoiongoza ndege hiyo, huku kituo cha mwisho cha safari hiyo ya majaribio kikiwa Abu Dhabi.
Rubani Andre Borschberg amenukuliwa akisema safari ya saa chache kabla ya kutua mjini Cairo ndiyo ilikuwa na changamoto zaidi kwani kwa mara ya kwanza betri ya ndege hiyo ilikuwa imeshuka hadi asilimia 30 pekee.
Huko ndiko mpango huo wa majaribio wa ndege hiyo ya sola ulianza hapo 2015.
Marubani hao Piccard na Borschberg awali walikuwa wakifanyakazi katika mradi wa sola uitwao Solar Impulse kwa muda wa zaidi ya miaka 10.
Japo ni safari ya polepole ndege hiyo imeweza kuvuka anga zaidi ya nchi 7 nyinginezo zikiwa ni zile zilizo na shughuli nyingi za ndege za usafiri wa umma.
Ni mradi ambao kufikia sasa umegharimu $100 millioni, tangu 2002 lakini lengo la utafiti huu ni kuwa huenda hatimaye gharama kama hiyo itakuwa ndogo ikilinganishwa na gharama ya harakati za kukabiliana na changamoto za kuongezeka kwa hali ya uchafuzi wa hewa kutokana na usafiri wa ndege nyingi unaotumia kawi ya mafuta.
No comments:
Post a Comment