Mkenya aliyedandia helikopta asimulia.
Bwana huyo alidandia licha ya maafisa wa usalama kuwazuia watu waliowasili kuona maiti.
Mwanamume huyo ambaye amebandikwa jina la mwigizaji, James Bond, aliwasili jijini Nairobi leo akiwa na furaha baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.
‘’Nimefurahi sana, nilihisi raha tofauti na kudandia ndege ambapo niliumia kutokana na upepo mkali angani,’’ alisema.
“Bado nahisi kuwa sijapata nafuu kabisa. Niliumia kwa sababu niliruka takriban mita kumi na moja kutoka hewani baada ya kushikilia ndege kwa muda.
Tofauti na safari yake ya awali juu ya ndege, ambapo alipanda kwa hiari wakati huu, ilikuwa vigumu kumshawishi Swaleh kusafiri kwa ndege.
“Nimeingiwa na woga tangu ajali hiyo, na sipendi tena ndege, alieleleza.
Bi Evelyne Namusya, mamake Swaleh waliosafiri naye hadi Nairobi, alieleza furaha ya kusafiri kupitia ndege akiwa na mwanawe.
"Hii ni mara yetu ya kwanza kusafiri kwa ndege na ninafuraha sana. Namshukuru mdhamini Joseph kwa kutuwezesha tufanikishe ndoto hii.”
No comments:
Post a Comment