Wednesday, April 6, 2016

JESHI LA POLISI TANGA LATOA SIKU 60 KUHAKIKI SILAHA



Tangakumekuchablog
Tanga, KAMANDA wa Polisi Mkoani Tanga, Leonard Poul, ametoa siku 60 kwa wamiliki wa silaha kuhakiki silaha zao na kuwataka wananchi kutoa taarifa za watu wanaomiliki silaha kinyume na sheria.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Poul aliwataka wamiliki wa silaha  kufanya hivyo kabla ya muda uliowekwa kumalizuika na kusema kuwa yoyote ambaye hatahakiki atachukuliwa kama mhalifu.
Alisema kufanya hivyo ni kuzuia matukio ya kihalifu ambayo yamekuwa yakihuisishwa na matumizi ya silaha ambao kuna baadhi ya watu ambao sio waadilifu silaha zao zimekuwa zikihusishwa.
“Natoa agizo kwa wamiliki wa silaha Tanga kuhakiki silaha zao kabla ya siku sitini, ambaye hatafa hivyo na silaha yake kuifungia ndani tutamchukulia kama mhalifu” alisema Poul na kuongeza
“Niwatake wananchi kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama kwa yoyote ambaye anamiliki silaha kinyume na sheria au kukaidi agizo la uhakiki” alisema
Kamanda aliwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya usalama kuhakikisha kila ambaye anamiliki silaha anatii agizo hilo ikiwa na pamoja na kuwafichua wamiliki haramu wa silaha.
Aliwataka kila mmoja kwa nafasi yake na eneo analoishi kutoa ushirikiano wa kuwabaini wamiliki wa silaha na kutoa taarifa ili kuweza kuwabaini wamiliki haramu wa silaha.
Akizungumzia usalama Mkoani hapa, Kamanda Poul alisema Mkoa huo uko na usalama na kuwataka wananchi wanaoishi mpakani mwa Horohoro na Mombasa Kenya kuacha kushirikiana na wafanyabishara wa magendo.
Alisema kuna baadhi ya watu wanaoishi mpakani wamekuwa wakishirikiana na wafanyabiashara wa magendo hivyo kuwataka kuacha kufanya hivyo kwani msako wa kuwabaini unaandaliwa.
‘Tunatambua kuwa kuna baadhi ya watu wamekuwa wakishirikiana na wafanyabiashara wa magendo na wapitishaji wa mihadarati, tunasema tabia hiyo ikomeshwe na dawa yao iko jikoni” alisema kamanda
Alisema polisi itafanya msako katika njia za panya ambazo wafanyabiashara wa magendo wamekuwa wakipitishia pamoja na majumba ambayo huhifadhi hivyo kutoa agizo yoyote ambaye atabainika atachukuliwa sheria.
                                         Mwisho

No comments:

Post a Comment