Samatta Atupia cha Tatu Ubelgiji
Jana usiku Samatta amerithibitisha hilo baada ya kupachika bao la tatu dakika ya 77 baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Nikolaos Karelis kwenye mechi yao dhidi ya KV Oostende.
Samatta alifunga bao hilo baada ya kutumia vyema pasi ya mshambuliaji wa kimataifa wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo Neeskens Kebano. Goli hilo linakuwa goli la tatu kwa Samatta toka ajiunge na klabu ya KRC Genk. Mpaka dakika ya mwisho KRC Genk 4-0 KV Oostende.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog

No comments:
Post a Comment