Wednesday, March 11, 2015

ANA MIEZI 11 HAPATI USINGIZI BAADA YA KUJIFUNGUA

Umeisikia hii ya msichana kukosa usingizi kwa miezi 11 baada ya kujifungua? 

girlMsichana mmoja amelalamika kwamba amekuwa akihangaika kwa muda mrefu kutafuta dawa itakayomsaidia kupata usingizi tatizo ambalo alilipata baada ya kujifungua.
Binti huyo amesema kuwa  hakuwa na tatizo lolote na alikuwa akiishi vizuri na kufanya shughuli zake kama kawaida, lakini baada ya kujifungua amejikuta na tatizo la kukosa usingizi wakati wote na kumfanya ashindwe kulala kwa miezi kumi na moja kwa sasa na mwili wake hausikii wala kuhisi kitu chochote.
Kutokana na tatizo hilo aliamua kwenda Hospitali na kuambiwa kuwa ana tatizo la kurukwa akili, akapatiwa dawa alizotumia kwa muda mrefu lakini bado hapati usingizi, kutokana na tatizo hilo lililomfanya aishi kwa tabu kuna wakati alijaribu kujiua zaidi ya mara tatu lakini ndugu zake walimuokoa na kwa sasa anahudhuria Kanisani kwa ajili ya kufanyiwa maombezi.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment