Tuesday, March 10, 2015

ARSENAL 2 MANCHESTER UNITED 1

Matokeo ya Arsenal vs Manchester United yasikupite mtu wangu… (Pichaz)

roon2Timu ya Arsenal usiku wa kuamkia leo iliendeleza kibarua chake cha kusaka tiketi ya kutinga hatua ya fainali katika mashindano ya kombe la FA baada ya kuvaana na mahasimu wao wa kihistoria, Manchester United kwenye uwanja wa nyumbani wa wakali hao wa Old Trafford.
Katika mchezo huo Arsenal ilifanikiwa kutinga nusu fainali ya kombe hilo baada ya kuilaza Manchester United kwa ushindi wa magoli 2-1.roon3
 Mchezaji wa zamani wa Man United, Danny Welbeck aliifungia Arsenal bao la ushindi katika dakika ya 61.
roon4Arsenal ndio walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 25 ya mchezo kupitia kwa mshambuliaji wao Nacho Monreal na baadaye Man U wakasawazisha dakika ya 29 kupitia kwa nahodha wao Wayne Rooney kabla ya Welbeck kuhitimisha ushindi.
roon5Angel Di Maria alitolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 77 baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano kwa kumsukuma Michael Oliver.
diNitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment