Tangakumekuchablog
Tanga,
MWENYEKITI wa CCM Wilaya ya Tanga, Kassim Mbuguni, ameutaka Umoja wa Madereva
wa Bajaj na Pikipiki (Moperoo) kuwasimamisha uanachama madereva wanaotumia
vilevi wakati wakiwa katika kazi lengo likiwa ni kupunguza ajali za barabarani.
Akizungumza katika uzinduzi wa ofisi
ya Umoja wa Madereva wa Pikipiki na Bajaj leo, Mbuguni alisema kuna baadhi ya
madereva ambao hawathamini kazi yao na badala yake wamekuwa wakitumia vilevi
wakati wakiwa kazini.
Alisema tabia hiyo imekuwa
ikijengeka kwa baadhi ya madereva ambao wameivamia kazi hiyo na kushindwa
kuithamini na hivyo kuutaka umoja huo kufanya kampeni ya kila dereva katika
maegesho ya pikipiki zao.
“Sekta ya usafirishaji abiria
bodaboda imekuwa kwa kasi na vijana wengi wamekuwa kimbilio---ila kuna baadhi
yake wameivamia na hawakupitia mafunzo ya udereva “alisema Mbuguni na kuongeza
“Bodaboda kwa sasa ni kazi yenye heshima tofauti na zamani wengi
walikuwa hawajui wajibu wao na kudhani kama ni nguvu kazi kama nyengine---sasa
mtu anavaa suti yake safi au sare yake akiwa nadhifu” alisema
Aliwataka kudumisha umoja na
mshikamano na matatizo madogo madogo yamelizwe kwa taratibu na kuwataka kuwa na
mawasuiliano na viongozi wao pamoja na walezi wa taasisi na vyama nyengine.
Akizungumza katika hafla hiyo fupi,
Mwenyekiti wa Moperoo, Silas Stivin, alimelitaka jehi la polisi kuwapatia redio
za upepo (Radio Coll) ili kuweza kuwasiliana na wenzao wakati wa kazini na hasa
wanaokodishwa kutoka nje ya mji.
Alisema maderava wengi wamekuwa
wakifanya kazi zao kwa hofu ya kutekwa na kuibiwa pikipiki kutokana na kutokuwa na mawasiliano na wenzao
katika vituo.
Alisema kuwepo kwa utaratibu huo
utasaidia kwa kiwango kikubwa kutokomeza utekaji na wizi wa pikipiki jambo
ambalo pia watakuwa wanafanya kazi kwa amani hata katika mazingira ya
kuogopesha.
“Kutokana na sekta ya usafirishaji
abiria kukua tunaomba Serikali kupitia
polisi kutupatia radio za upepo ili kuweza kuwasiliana kituo kimoja na chengine
ikiwa na pamoja na kufanya kazi kwa
amani” alisema Stivin
Aliwataka madereva hao kuheshimu
sheria za barabani pamoja na kuwa na lugha nzuri kwa wateja wao jambo ambalo
litaweza kuongeza kipato na uaminifu na
kuwa na uhakika wa kufanya kazi.
Mwis ho
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tanga, Kassimu Mbuguni (kulia)akikata utepe kufungua ofisi ya Umoja wa Madereva wa Bajaj na Pikipiki Tanga(Moperoo) iliyoko kata ya Mtupie Tanga jana, kushoo ni kamanda wa polisi wa usalama barabarani Tanga, Abdi Issango
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tanga, Kassim Mbuguni pamoja na Madiwani na wenyeviti wa Serikali za mitaa kata ya Mtupie halmashauri ya jiji la Tanga wakiangalia pikipiki 10 zilizonunuliwa na Umoja wa Madereva Tanga (Mopetoo) ikiwa ni sehemu ya umoja huo kukopeshana ili kujikwamua na maisha tukio lililofanyika leo.





No comments:
Post a Comment