MAHAKAMA TANGA YAZINDUA BODI YA PAROLE
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Magalula Said
Magalula amewataka wajumbe wa Bodi ya Paroli Mkoa kutenda kazi kwa kufuata kanuni na taratibu
zilizowekwa ili haki itendeke na kuepuka ushawishi wa namna yeyote katika
kupokea na kuomba rushwa.
Hayo
yamesemwa wakati wa
uzindua rasmi Bodi ya Parole Mkoa tukio lililofanyika katika ofisi za
Magereza Mkoani humo.
Alisema Lengo la Bodi hiyo ni kuwajadili
wafungwa wenye sifa za kuweza kuachiliwa
huru baada ya kutimiza vigezo ambavyo vimeainishwa kwenye sheria namba 25 ya Paroli ya mwaka 1994 na kufanyiwa
mabadiliko mwaka 2002.
Alisema sheria husika imeweza
kuanisha ni aina gani ya makosa ambayo mfungwa anaweza kupata fursa ya kuingia
kwenye mpango wa Paroli . Pamoja na makosa hayo mfungwa hawezi kuingizwa kwenye
utaratibu wa Paroli endapo amepatikana na kosa la unyang'anyi wa silaha, madawa
ya kulevya, kulawiti, kubaka na mauaji ya kukusudia.
Akiwasilisha taarifa ya
utekelezaji wa sheria ya parole tangu utekelezaji wake mwaka 2003, Mkuu wa
Magereza Mkoa wa Tanga Kamishina Agustino Mboje amesema tayari wafungwa 331
wameshaachiliwa huru kwa utaratibu wa parole, wafungwa 305 wamemaliza vifungo
vyao salama na wafungwa 26 bado wanaendelea na vifungo vyao kwa utaratibu huu.
Licha ya kuwepo na mpango
huu wa kupunguza msongamano wa wafungwa gerezani lakini bado wafungwa wengi
wameshindwa kunufaika na utaratibu wa Paroli kutokana na kutotimiza masharti ya
parole.
Maafisa wa Magereza wakimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa
Tanga, Magalula Said Magalula
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga Kam. Augostino Mboje
akitoa taarifa ya utekelezaji wa sheria ya Parole katika Mkoa wa Tanga
Baadhi ya wajumbe na Maafisa wa magereza wakati wa
uzinduzi
No comments:
Post a Comment