Idadi ya waliofariki kwenye mafuriko ya Kahama, waliokosa makazi na jinsi ya kuwasaidia.
Mpaka March 6 leo 2015 serikali ilithibitisha
kwamba waliofariki wamefikia 45 ambapo waliojeruhiwa walikua wanaendelea
kupatiwa matibabu huku mkurugenzi Idara ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu
Nyanchenghe Nanai akisema ni zaidi ya watu 70 hawana makazi na nyumba
zilizoharibiwa ni 137.
Hiyo imeilazimu serikali kupeleka msaada wa
haraka ili kuwanusuru waathirika wa mafuriko hayo ambapo pia Waziri
mkuu amekwenda kuwapa pole na bado mkurugenzi huyu amesema bado misaada
inahitajika kwa ajili ya waathirika sanasana ya makazi na chakula.
Watu 574 hawana sehemu ya kuishi ambapo
waliojeruhiwa ni 82, watu waliokosa makazi wanaishi kwenye shule za
msingi Mwakata, Numbi na Mwaguguma ambazo imebidi zifungwe kwa muda
kutoa huduma za masomo.
No comments:
Post a Comment