Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com
Wednesday, March 11, 2015
MWANASHERIA WA ZITTO KABWE NGANGARI
Info ya mwisho kusikika inahusu taarifa zilizochukua headline jana kwenye vyombo vya habari juu ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe,
baada ya kutolewa kwa hukumu ya kesi aliyokuwa ameifungua kupinga
CHADEMA kujadili uwanachama wake, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lisu amesema, wamemshinda kesi aliyofungua na kutokana na katiba ya chama hicho Zitto sio mwanachama wa chama hicho tena.
Wakili za Zitto, Alberto Msando
amesema kilichotokea sio hukumu kwasababu kesi ya msingi bado
haijasikilizwa, ila kulikuwa na mapingamizi ya awali kuhusu uhalali wa
kesi ya msingi kuwepo mahakamani ndicho kitu Mahakama imetolea maamuzi
kwamba, pingamizi la awali linamantiki kuwa kesi hiyo ilitakiwa
ifunguliwe Mahakama ya chini na sio hukumu kama inavyosemekana kwa kuwa,
kesi ya msingi bado haijasikilizwa na hawakuwa na taarifa za kesi hiyo
kusomwa jana, kwa sasa wanaangalia nini cha kufanya ili waweze
kujiridhisha, kuhusu kuvuliwa uwanachama wake amesema tamko hilo
limewasikitisha na halijafata utaratibu lakini kunauwezo wa kupeleka
swala hilo Mahakamani na kuomba zuio la muda hadi kesi itakaposikilizwa
ili aendelee kuwa mwanachama.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment