Thursday, March 5, 2015

BABA MWENYE NYUMBA ADAIWA KUMBAKA BINTI WAKE WA NDANI

 Utata wa taarifa ya msichana wa kazi kuingiliwa na baba mwenye nyumba 

domestic_violence1
Malalamiko kuhusu baba mwenye nyumba kushutumiwa kumbaka msichana wake wa kazi baada ya kumlaghai ndiyo ishu ambayo imehusika kwenye mitandao ya kijamii leo.
Ishu hiyo imetokea Chang’ombe jijini Dar es Salaam ambapo majirani walitishia kuandamana kwa kuwa baba huyo anashutumiwa lakini hakuna hatua yoyote ya kesheria iliyochukuliwa.
Majirani wamesema kuwa binti huyo aliwafuata akiwa analia na kulalamika kuwa tumbo linamuuma kutokana na baba huyo kumlaghai na kisha kumbaka, wakaamua kumpeleka Polisi ambako walipewa PF3 na kumpeleka katika Hospitali ya Temeke ambako alilazwa.
Mwenyekiti wa eneo hilo amesema alipata taarifa baada ya mke wa baba anayetuhumiwa kwenda Hospitali kumchukua binti huyo lakini walimkatalia na kumtaka aende na barua kutoka ofisi za Serikali.
Daktari aliyemfanyia uchunguzi amesema hakuna dalili ya msichana huyo kuingiliwa, majirani hao wameamua kumpeleka ofisi za ustawi wa jamii ili wafanye uchunguzi zaidi.
Mke wa mwanaume huyo amesema alipigiwa simu na mpangaji mwenzake akimpa taarifa hizo lakini alipomuuliza mume wake kama alikataa kufanya kitendo hicho.
Hutopitwa na habari yoyote inayonifikia na niko tayari kukutumia wakati wowowte kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment