Thursday, March 5, 2015

BALOZI WA MAREKANI NCHINI KOREA YA KUSINI ASHAMBULIWA

BALOZI WA MAREKANI ASHAMBULIWA KOREA KUSINI
Balozi Mark Lippet wa Marekani nchini Korea ya Kusini akiwa na majeraha baada ya kushambuliwa  kwa kisu usoni na pia katika kifundo cha mkono wake na mshambuliaji aliyekuwa akibwata kuhusiana na suala la kugawanywa kwa kipande cha ardhi ya jumuiya yao.
Mara tu baada ya shambulio hilo Rais wa Marekani Barack Obama amemtakia uponaji wa haraka msaidizi wake wa zamani Mark Lippert akimuombea uponaji wa haraka baada tu ya shambulio lililofanywa wakati wa hotuba ya asubuhi.
Balozi huyo mwenye umri wa miaka 42 alikimbizwa hospitalini ambako alifanyiwa upasuaji wa zaidi ya masaa mawili ingawa madaktari wamethibitisha majeraha yake hayahatarishi maisha yake. Chanzo BBC
Hutopitwa na habari yoyote inayofikia wakati wowte kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment