Tanga, KAMPUNI ya
usafirishaji abiria, FREYS COACH, imeanzisha safari zake kutoka Tanga, Moshi
hadi Singida kwa mabasi yake mapya (LUXURY BUS) ambayo mbali ya huduma zake za
vinywaji, vitafunwa na viburudisho pia mteja anaweza kukata tikiti yake kwa njia ya
mtandao.
Mapinduzi haya mapya katika sekta ya usafirishaji abiria imepokelewa kwa mikono miwili na watu mbalimbali na kuishauri pia
kuweka njia tofauti ili kuweza kupata huduma kama hizo kwa Mikoa mengine.
Akizungumza na waandishi wa habari
leo wakati wa uzinduzi wa usafiri huo, Kaimu Mkurugenzi wa Freys Coach, Hanfrey
Skauki, amewataka wakazi wa Tanga, Moshi, Arusha na maeneo mengine kuwa kampuni
hiyo imedhamiria kuleta mageuzi katika sekta ya usafirishaji abiria.
Alisema usafiri huo ambao utaanza
rasmi kesho asubuhi kwa wakazi wa Tanga na Mkoa wa Arusha kwa magari hayo
kupishana na kudai kuwa huduma zote za kiutu zinapatikana wakati wote wa
safari.
“Kampuni ya Freys imedhamiria kuleta
mageuzi katika usafirishaji abiria kwa kuwaletea magari ya kisasa (luxury
bus)-----tunawaomba abiria wa Mikoa yote kutuunga mkono siku zote” alisema
Hanfrey
Akifafanua zaidi juu usafiri huo,
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema ofisi zake kwa Tanga ziko barabara ya 12 mkabala
na kituo cha mafuta au stendi ya zamani na kwa upande wa Moshi huduma
zinapatikana ofisi zilizopo kituo huko.
Alisema kwa huduma za kukata tikiti
kwa kwa wateja wa mbali na ofisi hizo wanaweza kutuma kwa njia ya mtandao wa
simu , 0674 124723 bila kujali eneo na Mkoa aliko.
Akitoa shukrani zake mara baada ya
taarifa hiyo, Mkazi wa Mikanjuni, Shembilu Chambega, alisema ujio wa magari hayo itakuwa
mapinduzi makubwa kwani kwa miaka mingi walikuwa wakisafiri kwa kutumia
magari ambayo hukumbana na kero nyingi zikiwemo joto kali ndani ya gari na kuseganasegana.(Msegomsego)
Akitoa ushauri wake aliitaka kampuni
hiyo mbali ya huduma nzuri ambazo wanatoa wakati wa safari mwanzo hadi mwisho
kukumbuka kuanzisha pia safari za Dar es Salaam.
Kwa maelezo zaidi wasiliana nao kwa simu 0674 124723, 0655 157163 au 0655 9029292 ofisini
Mwisho









No comments:
Post a Comment