Friday, March 13, 2015

MENGINE MAPYA KWA OSCAR PISTORIUS

Kingine kuhusu rufaa ya Oscar Pistorius mahakamani Afrika Kusini.

pistoOctoba 21 2014 mwanariadha mlemavu wa miguu Oscar Pistorius alianza kutumikia kifungo cha miaka mitano jela baada ya kukutwa na hatia ya kumuua aliyekuwa mpenzi wake Reeva Steenkamp kwa kumpiga risasi.
Tangu aanze kutumikia kifungo mwanariadha huyo aliingia kwenye headlines baada ya kukata rufaa ambayo ilikataliwa pia ishu ya kupunguziwa masharti magumu kwa kuruhusiwa kuonana na ndugu zake pamoja na kuzungumza kwa simu lakini kingine ambacho kilitokea hivi karibuni ni ishu ya yeye kukataa chakula cha gerezani akihofia uhai wake kwa kuwekea sumu na wenzake.
oscarStori mpya kwa sasa ni mawakili wa mwanariadha huyo kugomea rufaa kuhusu hatua ya mahakama ya kumuondolea mashtaka ya mauaji.
Jaji Thokozile Masipa ametoa uamuzi katika mahakama ya Johannesburg kwamba ombi hilo likataliwe.
Baada ya kusikizwa kwa rufaa hiyo jaji Masipa alisema kuwa maelezo hayamruhusu kusikiza ombi hilo ama hata kulitupilia mbali.
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment