Mdahalo huo ambao ulikuwa wa kusisimua na kuwavutia watu
waliohudhuria ulikuwa ukionyweshwa moja kwa moja na kituo cha Televisheni cha
Tanga Tv na wengi wao wameiunga mkono na kuwataka wananchi kuipokea.
Katika mdahalo kulikuwa na vionjo
vya hoja za kisheria ambapo wengi walikuwa wanajiuliza kuwa wanafunzi hao
wamekuwa wakifundishwa somo la sheria kituo hapo baada ya kila mmoja kutoa hoja
za kisheria juu ya Katiba Pendekezwa.
“Toka mchakato wa kuandikwa Katika
Mpya, Rasimu na sasa Katiba Pendekezwa wananchi walikuwa wakishiriki kwa hali
na mali ili tu kuweza kupata Katiba iliyo bora---kuelekea Katiba
Pendekezwa makundi yote yatashirikishwa
kama ilivyokuwa hapo nyuma? Na kama sio hivyo Katika itakayokuja itakuwa ni ile
inayotakiwa na wananchi” aliuliza Lusekelo Emeiy
Emeiy aliwataka wananchi kuipitia
Katiba Pendekezwa kifungu kimoja baada ya chengine na kuweza kutoa michango yao
kutoka moyoni na kuacha kusemea pembeni na kupoteza haki zao kikatiba.
Kwa upende wake, Mwanafunzi Sakina Mshangama, ametaka Tume ya Mabadiliko Katiba Mpya kuisambaza Katika Pendekezwa na
wananchi kuweza kuipitia ili kuweza kutumika katika uchaguzi mkuu mwaka huu.
Alisema Watanzania wengi wangependa
kuona wanaingia katika uchaguzi mkuu wakiwa na Katiba Mpya ambayo pia itawapa nafasi wagombea nafasi mbalimbali za kuongoza kuipitia.
“Binafsi na watanzania wengi
tungependa kuona tunaingia uchaguzi mkuu tukiwa na Katiba Mpya----hii pia
itawapa fursa wa nafasi za kugombea kuipitia na kujua miongozo yao” alisema
Mshangama
Kutokana na kivutio cha Mdahalo huo
kunoga, watazamaji wa Televisheni na waliohudhuria waliomba kufanyika tena
mdahalo mwengine kwani mbali ya kufaidika kwa mambo ambayo walikuwa hawayajui
lakini pia umeibua Changamoto, Vuguvuvu, Hamasa , Utayari wa kuipokea Katiba
Pendekezwa na Katiba yenyewe.
Mwisho

Mwanafuzi wa kituo cha Elimu cha New Age Centre Tanga, Lussekelo Emeiy akizungumza katika mdahalo wa katiba ya Katiba Pendekezwa uliofanyika Tanga.
Mwanafunzi wa kituo cha Elimu cha New Age, Sakina Mshangama akizungumza katika mdahalo wa katiba Pendekezwa uliofanyika Tanga.
Wanafunzi wa kituo cha Elimu cha New Age Tanga, wakifuatilia mdahalo wa Katiba Pendekezwa uliofanyika Tanga
Tunafuatilia kwa makini, ndivyo wanavyoonekana wanafunzi wa kituo cha Elimu cha New Age Tanga.

















No comments:
Post a Comment