Friday, March 6, 2015

MWARABU WA DIAMOND KUMBE NI MWANAMIELEKA?

March 6, TID kupiga show, Utaratibu mpya kwenye muziki, bodyguard wa Diamond kwenye mieleka

entertainment_news_stopimageInfo ya kwanza kusikika  March 6, ni  ishu ya bodyguard wa msanii Diamond Platnumz anayefahamika kama Mwarabu Suleimani ambaye alikuwa Tajikistan kushiriki kwenye mashindano ya kupigana ya mieleka ambayo yalikuwa na washiriki kutoka mataifa mbalimbali.
LIVINGSTONE MKOI (3) (2)Mwarabu amesema mchezo wa kwanza alicheza na jamaa wa Italy na game ya pili alicheza na jamaa kutoka Iran lakini matokeo hayakuwa mabaya tofauti na alivyotegemea, siku mbili kabla ya pambano la mwisho alipata jeraha mguuni wakati akifanya mazoezi na kupoteza michezo miwili.
tid4Weekend hii msanii TID kwa kushirikiana na Radar Entertainment pamoja na msanii Nazizi kutoka Kenya watafanya show Club Bilz, akizungumza kwenye 255 TID amesema amejipanga vema kwa kuwa ni show yake ya kwanza mwaka huu na kutakuwa na wasanii mabalimbali pamoja na surprise za kutosha pamoja na uzinduzi wa video ya msanii Masai Sharo.
nikiStory ya mwisho kusikika inahusu uzinduzi uliofanyika jana wa program mpya chini ya msimamizi wa hakimiliki wa Afrika Mashariki (East African Copyright Management) ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba.
Utaratibu mpya ambao utasimamiwa na program hiyo ni ishu ya wasanii kulipwa na vyombo vya habari vinavyocheza kazi zao, msanii Nikki Wa Pili ni miongoni mwa wasanii waliohudhuria ambaye amesema itasaidia msanii kupata matunda ya kazi anayoifanya.

No comments:

Post a Comment