TANGAKUMEKUCHABLOG
Tanga,JESHI la Polisi Tanga limesema
litafanya msako katika kumbi na madanguro ambayo yanatajwa kuendesha
biashara ya kujiuza na kuwataka wananchi kutoa taarifa za majumba
yanayoendesha biashara hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari
ofisini kwake jana, Kaimu kamanda wa polisi Mkoani Tanga, Juma Ndaki, alisema
polisi itafanya msako huo baada ya taarifa kutoka kwa wananchi juu ya kuwepo
kwa tabia hiyo.
Alisema polisi itafanya msako katika
kumbi na majengo ambayo yanadhaniwa kuweko kwa biashara hiyo haramu
ambayo awali waliweza kuitokomeza na sasa kuibuka tena.
“Kama kweli biashara hiyo ipo katika
maeneo hayo ambayo yanatajwa basi niwahakikishie wakazi wa Tanga kuwa polisi
itaitokomeza-----msako huo utaenda sambamba na kuwachukulia hatua watu
wanaojihusisha nayo” alisema Ndaki na kuongeza
“Tanga haiko na utamaduni huo kwani
kama kweli tetesi zinazotajwa kuwepo na zikiachiwa zinaweza kuleta athari kwani
hata watoto wadogo wanaweza kujitumbukiza katika mkumbo huo” alisema
Akizungumzia kuhusu watu wanaofanya
biashara haramu ya mihadarati na upitishaji wa wahamiaji haramu, kamanda Ndaki
alisema polisi itazidisha doria usiku na mchana katika mpaka wa Horohoro.
Alisema kwa sasa wameweza kuzuia
mianya ya upitishaji wa mihadarati na wahamiaji haramu ila kuna baadhi ya watu
wamekuwa wakiibuka na kuwataka wakazi wanaoishi mpakani kuacha kushirikiana na
watu wa aina hiyo.
“Natoa agizo kwa wakazi wanaoishi
mipakani kuacha kushirikiana na watu wanaofanya biashara za magendo na
upitishaji wahamiaji haramu-----tutaendesha msako na tutakaemgundua mahakamani”
alisema Ndaki
Alisema msako huo utahusisha askari
polisi na polisi jamii ambao watakuwa wakifanya kazi usiku na mchana na hivyo
kuwataka wakazi wa maeneo hayo kuacha kujihusisha na watu wenye tabia hiyo.
No comments:
Post a Comment