Siku ya wanawake Duniani Rais wa Korea Kusini hakukosa zawadi ya kuwapa wanajeshi wanawake
Katika mataifa ambayo hayako kwenye uhusiano mzuri duniani ni Marekani na Korea Kusini, Kim Jong-Un
ambaye ni Rais wa Korea Kusini amekuwa akitajwa kama mmoja ya viongozi
ambao hawatabiriki kwenye suala la maamuzi, anaamua chochote
atakachojisikia kwa wakati wowote.
Siku ya March 8 dunia nzima
ilisherehekea siku ya wanawake Duniani, watu wakapeleka zawadi kwa dada
zao, ndugu zao wa kike, lakini mlengwa mkubwa alikuwa mama.
Rais wa Korea nae alikuwa na zawadi kwa
wanajeshi wake wanawake ambao wako kwenye Kambi ya siri ya Jeshi la nchi
hiyo, katika ziara yake hiyo amegawa vitu kadhaa kwa wanajeshi hao
ikiwemo vipodozi vya wanawake kama vile poda na vingine.
Japo Kim hakukutana na wanajeshi hao
mmoja mmoja lakini mzigo wa zawadi hizo ulifikishwa kwa Mkuu wa Kambi
hiyo na kuagizwa kwamba ni zawadi ambazo zinatakiwa kumfikia kila
mwanamke ambaye yuke kwenye kambi hiyo.
Wewe ulimpa zawadi gani mama yako? Unaweza kuniandikia yako hapa lakini Rais Kim yeye katoa zake vipodozi.
No comments:
Post a Comment