Friday, March 13, 2015

TRA TANGA WAWAPIGA CHENGA WAFANYABIASHARA

Tanga, KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya  Wafanyabiashara Taifa, Silver Kiondo amekilalamikia kitendo cha Maofisa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga kutoka katika kikao cha Wafanyabiashara na kusema kitendo hicho kunamaanisha hakuna ushirikiano.

Hapo jana, kimefanyika kikao cha wafanyabiashara wenye maduka kujadili ongezeko la asilimia mia ya mapato pamoja na matumizi ya mashine ya kutolea risiti na hivyo kushindwa kujadili baada ya maofisa hao kutoka nje.

Akilizungumzia kitendo hicho, Katibu huyo amesema wafanyabiashara wataendelea kuiomba Serikali kuangalia upya ongezeko hilo sambamba na matumizi ya mashine vyenginevyo migomo ya nchi nzima itafanyika.

Akizungumzia Kikosi cha Uokozi cha Jeshi la Zimamoto kupita madukani na kukusanya kodi , amesema kitendo hicho ni hatari kwani kikosi hicho ni sawa na jeshi na hivyo wanaweza kutumia nguvu za kijeshi ili kujikusanyia pesa jwa nguvu.

Amesema kulazimishwa wafanyabiashara kuweka kifaa cha kuzimia moto madukani ni cha uonevu na hivyo kuitaka Serikali kufuta sheria hiyo kwani ni kuwanyonyoa wafanyabiashara kiuchumi.

"Kitendo cha Serikali kuruhusu kikosi cha Zimamoto na Uokozi kukusanya kodi za fere madukani ni hatari kwa usalama wa mfanyabiashara -----lile ni jeshi na watatumia mbinu za kijeshi kuhakikisha wanakusanya kodi " alisema Kiondo

Alisema kwa sasa Serikali inaonekana haina huruma kwa mfanyabiashara na wanataka kumkamua kila ambapo inaona ananufaika na hivyo kuitaka kulegeza masharti ili kuweza kufanya biashara na kuweza kulipa kodi bila mikwaruzo na maofisa TRA.

                                                  Mwisho

No comments:

Post a Comment