Niseme kwamba kama kweli Chadema inataka kuleta mageuzi ya
Kidemkrasia katika Uchagzu mkuu unaokuja imefanya uamuzi wa haraka
kumfukuza ndani ya chama kwani ni kiungo muhimu na yuko na ushawishi
mkubwa ndani na nje ya chama. Ushauri wangu ni vyema Zitto akabaki
Chadema na suluhu ifanyike kwani kujiunga na vyama ni kuwagawa wananchi.
Ali Juma Mkazi wa Manundu Korogwe Tanga.
Hawakumtendea haki Zitto na uamuzi waliochukua ni wa haraka
na inaweza kuwaletea doa Chadema hasa kuelekea uchaguzi mkuu mwaka
huu. kwani Zitto yuko na ushawishi kwa vijana na wazee. Ushauri wangu
kwa Zitto ni kuangalia upepo kwanza kwani Chama kikiyumba wanaweza
kumkaribisha na kujiunga na harakati zao za mageuzi. Fredy Muya, mkazi
wa Old Korogwe
Nashangazwa kuona
Zitto amefukuzwa kwani najua kila chama cha siasa kinamtaka hata CCM,
nisema wamempoteza mtu muhimu mwenye ushawishi ndani ya chama kwani kila
alipokuwa anaenda alikuwa anavuna wanachama na watu walikuwa
wanamsubiria. Ushauri wangu ni kwenda katika chama ambacho kitakuwa na
mvuto wa mageuzi na kuweza kupata nafasi ya kuongoza na kuweza kututetea
Bungeni hasa sisi vijana ambao hatuna ajira. Mtemi Juma mkazi wa Mtonga
Korogwe



No comments:
Post a Comment