Tuesday, February 10, 2015

AKAMATWA NA TANI MOJA KENYA

Jamaa mmoja amekamatwa akiwa anasafirisha bangi Kenya, huu utetezi wake ni story…

Jailed Man
Mtu mmoja amekamatwa akiwa anasafirisha bangi baada ya gari alilokuwa akisafirishia kupata ajali likiwa linatokea maeneo ya Busya kuelekea Nairobi, Polisi wakafanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo.
Bangi sio kitu ngumu hata tumbaku ni so expensive kushinda bangi… sasa bangi ngoja nikuambie hiyo tani moja tukinunua Uganda ama Tanzania tunanunua 50 buku na tunauza 100 buku, lakini saa hii hawa wakikushika wanakuambia one milion, sasa one milion ningekuwa nafanya hii kazi? Ningepata one milioni kwani mimi nitakuwa mjinga nikimbie njiani kila siku?“– alijitetea mtuhumiwa huyo.
Mtuhumiwa huyo ambaye amepelekwa rumande amekiri kufanya biashara hiyo kwa zaidi ya miaka kumi sasa likiwa ni tukio lililotokea siku chache baada ya watuhumiwa wengine kukamatwa na bangi katika maeneo hayo.

Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment