Jamaa aliyemuua rafiki yake na kumzika kwenye nyumba yake.
Taarifa zinasema kuwa mtuhumiwa alikuwa ameagizwa na marehemu ambae ni rafiki yake na kumpa shilingi milioni 35, amnunulie gari lakini hakufanya hivyo na alipoanza kumdai hela zake alimzungusha na siku moja alimpigia simu ili afate hela zake na alipofika alimuua na kisha kufukia mwili wake kwenye nyumba hiyo aliyokuwa amepanga.
Baada ya ndugu kumtafuta ndugu yao bila mafanikio walitoa taarifa Polisi na mtuhumiwa akakamatwa kutokana na kuwa na marehemu dakika za mwisho, baada ya kuhojiwa aliachiliwa kwa dhamana huku Polisi wakiendelea na uchunguzi ndipo walipokuja kumkamata tena na walipombana alikubali kuwa ameuwa na kuwaleta eneo alilokuwa anaishi na kuwaonyesha eneo ambalo alifukia mwili wa marehemu na kisha kusakafia.
Mjumbe wa mtaa huo amesema kuwa hawajawahi kusikia harufu wala kuhisi chochote walishangaa kuona Polisi wanakuja na mtuhumiwa na kuwaelekeza eneo hilo na kuanza kuchimba kwa kushirikiana na vijana wa eneo hilo na kuukuta mwili huo ukiwa umefungwa kwenye godoro huku badhi ya viungo kama miguu na mikono vikiwa vimekatwa na mwili huo ulionekana ulikuwa umechomwa moto.
No comments:
Post a Comment