Friday, February 6, 2015

MAAJABU, HEBU SIKIA

Anawapenda wote, anawahitaji wote na akafanya uamuzi huu ili asiwapoteze…

self-loveWivu ni chanzo cha migogoro katika uhusiano pengine jamaa hawa wawili hawana wivu kabisa baada ya kukubaliana kuishi kinyumba na mwanamke mmoja huko Zimbabwe.
Mwanamke huyo Mlambo amesema kuwa anaenjoy maisha kwa kuishi na wanaumea hao wawili katika nyumba moja na hawezi kuishi na mmoja kwa kuwa anawapenda wote wawili na hayuko tayari kumpoteza hata mmoja.
Mlambo anaishi nyumba moja na jamaa hao Wesley Gora na Fungai Matandaudyi, amesema anawapenda wote wawili na kila mmoja anampenda kwa sababu tofauti, anachijitahidi kukifanya ni kuhakikisha hamkosei hata mmoja wao, wanaishi kwa furaha kwa sababu walikubaliana kuishi maisha hayo kwa kuheshimiana.
image20
Gora amesema kuwa mwanzo alikuwa na hasira alipogundua kuwa mke wake alikuwa na uhusiano na mtu mwingine, baadae aligundua kuwa mwanamke huyo anawapenda wote wawili, alikubali kuendelea naye.
Matandaudyi amesema walianza mahusiano miezi nane iliyopita alipogundua kua mpenzi wake ana uhusiano na Wesley walikaa na kuzungumza, wakakubaliana mpango wa kuendelea wote pamoja.
Hii unaionaje mtu wangu?
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment