Hivi unaweza kuacha CASH mezani kwako na ujumbe eti mwizi akiingia azichukue? Isome hii…
Hakuna mtu anayependa uhalifu hata
kidogo, lakini vipi unakutana na mtu ambaye anaacha pesa ndani ya nyumba
yake pamoja na ujumbe kwa mwizi yoyote ikitokea kaingia ndani ya nyumba
basi ajichukulie kiurahisi!
Nakusogezea kutoka China, wanandoa
wameacha hela kwenye meza kiasi cha Yuan 300 (sawa na sh. elfu 85 Tshs)
pamoja na ujumbe ambao unamtaarifu mwizi yoyote atakayeingia achukue
hela hizo.
Imekuwa kawaida yao kufanya hivyo,
safari hii walikuwa wakisafiri kwenda Shenzhen, Kusini mwa China safari
ambayo walipanga kukaa kwa miezi miwili.
Ujumbe waliouacha unasomeka hivi; “Najua
umehangaika sana mwaka huu. Lazima una hamu ya kuwaona wazazi wako,
chukua pesa hizi kakate ticket ya treni na uende kuwasalimia. Kama
ukirudi utafute kazi ya heshima“
Ujumbe wa wanandoa hao pamoja na cash waliyoiacha kwenye meza yao.
Mwaka 2010 waliwahi kusafiri na kuacha
pesa na ujumbe kama huo, waliporudi walikuta mlango umevunjwa na pesa
zimeibiwa lakini hakuna kitu chochote kingine ambacho kimeibiwa ndani ya
nyumba yao.
Hautopitwa na story yoyote inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com
No comments:
Post a Comment