Tuesday, February 10, 2015

NEWS FROM KENYA

Nimekuwekea mkusanyiko wa Habari kubwa mbili zilizoripotiwa na kituo cha Citizen TV kutoka Kenya

Highway_COWI_P5_highWatuhumiwa watatu wamefikishwa  katika Mahakama ya Kilimani Nairobi kwa  njama ya kufanya utapeli kampuni ya PAFCO ardhi yenye thamani ya shilingi milioni 338, ambapo inadaiwa kuwa watuhumiwa hao walitoa taarifa za uwongo ili kuweza kumiliki eneo hilo la ardhi.
Lidya Makena amejikuta akiwa na huzuni kubwa siku ya jumamosi ambapo ilikuwa siku ya kuzaliwa ya mpenzi wake wake baada ya mpenzi wake huyo Samuel Kimath ambaye alikuwa mlinzi wa Mbunge wa Kabete, George Muchai kuuawa na watu wasiojulikana.
Mbunge wa huyo George Muchai aliwahi kutamka kuwa kuna watu wana njama za kumuua japo hakuwataja, kitu ambacho kimeacha kitendawili kikubwa huku wabunge wa Kenya wakiitaka serikali kuwataja watu waliohusika na kifo hicho ambacho wamekihusisha na masuala ya kisiasa.
Hutopitwa na habari yoyote mtu wangu na niko tayari kukutumia wakati wowote kupia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment