Monday, February 9, 2015

TETESI ZA VANESSA NA SHAA KUTOKUWA NA UELEWANO YAZAGAA KATIKA MITANDAO

 Wasanii Vanessa Mdee na Shaa wazungumzia ishu ya dancers wao

DSC_0343
Shaa akiwa na dancers
Jumatatu ya February 9 nimekuwekea  ya leo ambayo inahusu tetesi za wasanii wakike Vanessa na Shaa kuonekana kutokuwa na maelewano kati yao katika show iliyofanyika hivi karibuni huku ikisemekana kuwa wanashare dancers hivyo kuwa na mvutano kila mmoja kutaka awe wa kwanza kuwatumia.
Soudy Brown alikutana na wasanii hao hivi karibuni wakiwa katika show kwa upande wa Shaa amesema kuwa hawana ugomvi wowote kwani wasanii wakike wako wachache kwa hiyo hawaoni haja ya kugombana.
DSC_0379
Vee Money akiwa na dancers
Vanessa nae amefunguka kuwa wanapeana support ili waweze kufika mbali, kuhusu dancers hao Vee amesema wako vizuri ndio maana wanawatumia wote kwa pamoja, hawana haja ya kugombana kwani watu wanataka kuwagombanisha ili washindwe kufanya muziki na kupotea kwenye ramani.

No comments:

Post a Comment