Wednesday, October 7, 2015

ASHINDA APOKWA MKANDA, MAAAJABU


Pamoja na kushinda ubingwa wa dunia, bondia Cosmas Cheka amerejea nchini bila ya mkanda.

Bondia huyo ambaye ni mdogo wake na bingwa mwingine wa Francis Cheka amerejea nchini bila ya mkanda huo.
Cheka amemtwanga bondia wa Thailand na kutwaa ubingwa wa uzito mwepesi wa WBO, lakini wenyeji wakaamua kutompa mkanda.
Taarifa zinaeleza, promota alionekana kukerwa na Cheka kumpiga bondia wao hadi kufikia uamuzi wa kumnyima.

Lakini juhudi zimekuwa zikifanyika kuwasiliana na WBO kuhakikisha mkanda huo unatumwa nchini.
Kwa habari matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment