Wednesday, October 7, 2015

JOSE MOURINHO HATARINI KUFUNGASHIWA VIRAGO VYAKE

Ikitokea Jose Mourihno kafukuzwa Chelsea, hiki ndio kiwango cha pesa atakacholipwa…

Mabingwa wa ligi kuu England Chelsea imepata matokeo mabaya mfululizo na kusababisha kuwa na sintofahamu juu ya kibarua cha kocha wao Jose Mourinho.
Pamoja na mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich kukanusha kumtimua kocha huyo lakini ukweli ni kwamba endapo watadhubutu kufanya hivyo itawalazimu kumlipa Kocha huyo kwa kumlipa kiasi cha Euro milioni 30.
Mourinho aliongezewa mkataba mwingine wa mwaka mmoja usiopungua Euro milioni 8.5 na kumfanya kuendelea kubaki ndani ya klabu hiyo hadi mwaka 2019.
Kutokana na matokeo mabaya wanayoyapata kwa sasa mabingwa hao watetezi wapo katika hatari ya kuukosa uchampion wa ligi hiyo msimu ujao.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment