Friday, October 16, 2015

MITANDAO YA KIJAMII NA TUKIO LA KUANGUKA HELKOPTA

Ajali

Ni stori iliyoanza kuchukua nafasi kubwa sana katika mitandao mbalimbali usiku wa kuamkia October 16 2015 headlines za siasa Tanzania zimetawaliwa na ajali ya Helikopta ambayo imeanguka kwenye mbuga ya Wanyama ya Selous ambapo Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alithibitisha kwamba mmoja wa waliokuwemo ndani ni Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM).
Leo baada ya saa kadhaa, mgombea Ubunge kupitia CCM jimbo la Ukonga, Jerry Silaa alipost picha ya Helicopter na kuandika maneno kuhusiana na ajali hiyo>>>”Baba yangu Capt.William Silaa akiwa na Mhe.Deo Filikunjombe na abiria wengine walipata matatizo ya engine ya helicopter 5Y-DKK jana jioni wakitokea Dar kuelekea Ludewa. Taarifa za mwisho ilionekana imeanguka kwenye msitu wa Selous. Hakuna mawasiliano ya simu. Usiku kucha vyombo vyote vya serikali vimeendelea na jitihada za kufika eneo la tukio na jitihada kubwa zaidi zinaendelea asubuhi hii >>> Jerry Silaa.
Nawaomba wote kuwa watulivu kwani jambo hili linahitaji umakini wa hali ya juu na ushirikiano wa taasisi nyingi za wizara tofauti. Tuwaombee wote Mungu awanusuru‘ – Jerry Silaa.
Baada ya hapo tukapata maelezo kutoka kwa Waziri wa Utalii na Maliasili, Lazaro Nyalandu akasema…>> “Tunaamini kwamba Mungu atafanya miujiza juhudi za kuwapata nafikiri muda si mrefu tunaweza tukafanikiwa, changamoto iliyosababisha watu wa msaada kuchelewa kufika kwenye eneo la ajali moja taarifa za hiyo ajali tulizipata wakati giza lilikuwa limeshaingia hilo la kwanza, la pili ajali hiyo imetokea katika kitalu cha wawindaji kinachojulikana kama R3 na walioshuhudia walikuwa katika kitalu R2 tofauti yao ni kwamba wametenganishwa na mto ambao unaenda kwa kasi halafu una mamba“>>> Waziri Nyalandu.
Sisi tulichokifanya kama Serikali ni kwamba tumetuma kikosi kimoja ambacho kilikuwa kina askari nane.. Mkuu wa Polisi Mkoa wa Morogoro pia naye akatuma askari kwenda kwenye eneo hilo la ajali, kwa hiyo lazima tufahamu kwanza helikopta ilipodondoka na tutambue kama kutakuwa na wale ambao watakuwa wamenusurika au wako wapi na leo Asubuhi tumetuma helikopta kuangalia kinachoendelea… Tunasubiri taarifa za huko watakaporudi kwani  sehemu ambayo walipo hakuna hata mawasiliano ya simu” >>> Waziri Lazaro Nyalandu. 
Taarifa tulizozipata kutoka kwa mashuhuda wa eneo hilo kwa wawindaji mahiri walipiga simu kwa njia ya Satelite na kusema kwamba wameona helikopta moja imeaguka msitu wa Selous kwenye  kitalu R3 mto Ruaha baada ya hapo wakaona moto kwa hiyo sisi kama Serikali tunaendelea kufanya uchunguzi wakina” – Lazaro Nyalandu.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment