Sunday, October 11, 2015

VITUKO KAMPENI , HII KALI YA MUSSA MBARUKU WA CUF



Tangakumekuchablog
Tanga, MGOMBEA Ubunge jimbo la Tanga mjini kupitia Chama Cha Wananchi (CUF) Mussa Mbarouk, amesema mara hii hatokubali kuibiwa kura zake na atakae jaribu atakula ngumi kali Kama za Mike Tyson.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara juzi, kata ya Marungu juzi, Mussa alisema upole wake utaisha pale atakapobaini mtu kumuibia kura zake na tayari ameshanunua gloves za kuvaa mikononi.
Kauli hiyo iliamsha shangwe na vifiko kwa watu waliojazana uwanjani hapo na baadhi ya watu walimtaka mgombea huyo kutenga muda wake wa kufanya mazoezi kwani kuna watu wamezoea kuiba kura.
“Ndugu zangu  musinione mimi  mpole mpole mukadhani ni legelege----mimi nimeshapitia kila aina ya mazoezi yakiwemo ya kupigana mandonga ila sijabahatika tu kubeba mkanda” alisema Mussa na kuongeza
“Nipelekeeni salamu zangu kwa waizi wa kura na waambieni kuwa nimeshanunua gloves maalumu kwa kuwatwanga  na  ni kali zaidi ya Mike Tyson” alisema
Mussa alisema Push up za CCM haziwanyimi usingizi  na  kudai kuwa wamechelewa kwani wao sasa hivi wanafanya mazoezi ya kupasha  misuli kusubiri kusherehekea ushindi wa kimbunga.
Alisema ukiwaangalia hao wapigaji push up hawafikishi hata tano na kusema yoyote atakaefikisha kumi atampa mabata wawili  akafanye mboga nyumbani kwake.

Mussa alisema ushindi mwaka huu ni mweupe kuanzia Udiwani, Ubunge hadi Urais hivyo kuwataka wananchi kuwapatia kura nyingi  wagombea wa Ukawa  na kuwaonyesha CCM kuwa nchi hii sio masikini ila kuna watu wanaowapa umasikini wananchi.
Akizungumza katika mkutano ambao ulihudhuriwa na mgombea Udiwani wa Ngamiani Kati, Habib Mpa,(CUF) ,amedai mwaka huu chama hicho kiko na uhakika wa kuongoza halmashauri na kula kuku kwa mrija.
Alisema kwa mahesabu ya harakahara ni kuwa CUF itanyakua viti zaidi ya 20 hivyo kutaka kuwaonyesha wananchi kuwa maendeleo yalikuwa yakikwamishwa na madiwani wa CCM.
“Ndugu zangu wa Marungu kazeni buti na tumuombe Mungu isije tokea dharura mmoja wetu akakosa haki ya kupiga kura kwani CCM wanatuombea mabaya ili kura zetu zipungue lakini nawaomba tuwageuzie kibao iwe wao ili tule kuku kwa mrija” alisema Mpa
Mpa aliwataka wananchi wa kata ya Marungu kutofanya kosa kwa kumchagua mgombea mwengine asiekuwa wa CUF  kwa madai kuwa chama hicho kimechoka na hivyo kutakiwa kupumzishwa .
                                                  Mwisho

No comments:

Post a Comment