Wednesday, October 7, 2015

VITUKO MIKUTANO YA KAMPENI, -----------YANKUWA HAYO TENA ?



Tangakumekuchablog
Tanga, KATIBU wa Itikadi na Uenezi  wa CCM Wilaya ya Tanga, Lupassio Kapange, amemtaka mgombea Ubunge jimbo la Tanga, Omari Nundu kupeleka posa kwa mgombea Ubunge jimbo la Tanga na mgombea Udiwani kata ya Mwanzange wote kupitia CUF kwa madai kuwa hawana heshima.
Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni wa kumnadi Nundu  Leo, Kapange alisema kutokana na sheria ya dini ya dini ya Kiislamu kuruhusu muumini kuoa wake wanne, hivyo mgombea huyo nafasi yuko nayo hivyo kupelekea posa kwa mgombea wa Ubunge, Mussa Mbarouk na mgombea Udiwani kata ya Mwanzange, Rashid Jumbe.
Alisema wagombea hao katika mikutano wamekuwa wakitoa maneo yasiyofaa na ili kuweza kuleta heshima ni mgombea huyo Omari Nundu kupeleka posa na kuweza kuwa shemeji yao.
“Hawa watu wamekuwa wakimsema vibaya mgombea wetu kwani wanatambua kuwa hawawezi kushinda na ndio maana wanasema sema hovyo hovyo----sasa nakuomba mheshimiwa peleka posa waweze kukuheshimu” alisema Kapange na kuongeza
“Mheshimiwa najua wewe ni muislamu safi na umeshawahi kwenda hijja na uko na mke mmoja---kwa vile dini yako inakuruhusu kuoa mke zaidi ya mmoja hebu peleka posa kwa Mussa Mbarouk na Rashid Jumbe uwazibe midomo ya kusema sema” alisema
Akilijibu hilo jukwaani mara baada ya kupewa nafasi,  Omari Nundu, alisema hatoweza kupeleka posa kwa watu hao kwani yuko na kimwana ambaye hasikii wala haoni na ametua kwake.
Alisema hatokuwa tayari kupeleka posa kwa wagombea hao wa nafasi ya Ubunge na Udiwani wa Chama Cha Wananchi (CUF) kwani mke alienae amepoa licha ya ruhusa ya dini yake kuruhusu wake wanne.
“Niko na kimwana  anaenipendezesha na ndio maana nipo hapa na kila mmoja ananifurahia----siko tayari kupeleka posa kwa watu hao kwani nitakapotangazwa kuwa nimeshinda wote watakuja na kunipa mkono kwa heshima zote” alisema Nundu
Nundu aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura na kuwachagua wagombea wa CCM kwani kila alopewa dhamana ya kugombea ameaminiwa na hivyo kuwapa kura nyingi za ushindi.
                                              Mwisho

No comments:

Post a Comment