Tuesday, October 13, 2015

WAANDISHI WATAKIWA KUACHA KUSHABIKIA VYAMA

Tangakumekuchablog

Dar es Salaam, WAANDISHI wa habari wametakiwa kuzitumia kalamu zao kuwaelimisha wananchi juu ya haki na wajibu wa kupiga kura  na kuacha kushabikia mambo ambayo hayana nafasi kwa jamii.

Akizungumza katika mafunzo ya siku mbili yaliyoandaliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwa kushirikiana na BBC Media Group, mwandishi mkongwe nchini, Atilio Tigalile, aliwataka waandishi wa habari kuzitumia siku zilizobaki kuandika habari nyingi za uchaguzi.

Alisema kuna baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikishabikia habari za upande mmoja na hivyo kuvitaka kuacha kufanya hivyo na badala yake kuandika habari za pande zote mbili bila upendeleo na kuzipa nafasi kubwa habari za uchaguzi.

“Ni jambo la furaha na faraja kuona waandishi wengi mupo hapa kuzungumzia uchaguzi----niwatake kuandika habari kwa weledi na usahihi bila kupendelea chama” alisema na kuongeza

“Hebu jamani tuzitumilieni siku hizi chache kwa kuandika habari  za uchaguzi tena bila upendeleo----kuna vyombo vyengine hata havisemezeki wapo kwa ajili ya mtu mmoja tu na huko itakuwa ni kukiukwa kwa maadili” alisema

Akizungumzia kuhusu wamiliki wa vyombo vya habari  TV na magazeti , Tigalile aliwataka kuandika makala kwa wingi kuelimisha wananchi juu ya wajibu wa kupiga kura .

Alisema kuna kundi kubwa vijijini bado elimu ya kupiga kura  haijawafikia  na hivyo kuvitaka kuandaa makala mfululizo pamoja na habari katika siku chache zilizobaki.

“Sote tunatambua kuwa wananchi wa mashamba na vijijini ni wafungwa wa kupata habari  hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu October 25’ alisema na Tgalile

Alisema mwandishi makini ni yule ambaye habari  yake anaifanyia  kazi na  kuuliza watu zaidi ya watatu  na kudai kuwa huo ndio  ni uandishi mahiri na makini ambaio hauvunji maadili.

                                                          Mwisho

No comments:

Post a Comment