Taiwan yarusha kombora la kulipua meli kimakosa
Kombora hilo lilianguka katika maji ya kisiwa cha Penghu karibu na China lakini halikusababisha madhara yoyote.
Kisa hicho kinajiri wakati ambapo China inasheherekea maadhimisho ya miaka 95 tangu kuanzishwa kwa chama cha Kikomyunisti.
Alisema kuwa kisa hicho kinachunguzwa na kitaangaziwa vilivyo.
Haijulikani iwapo Bejing ilijulishwa.
Kombora hilo linaweza kurushwa umbali wa kilomita 300.China inaichukulia Taiwan kama mkoa wake uliojitenga.
BBC
No comments:
Post a Comment