Tangakumekuchablog
Tanga, WAFANYABIASHARA wa
Pikipiki maarufu kama bodaboda Tanga, wameitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) kuongeza muda wa usajili wa namba za pikipiki vyenginevyo watasitisha
utoaji wa huduma barabarani.
Wakizungumza katika kongamano la kujadili changamoto
zinazoikumba sekta hiyo, madereva hao wamesema muda uliowekwa wa kubadilisha
namba za pikipiki ni mdogo na hivyo kutaka kuongezwa.
Walisema endapo Mamlaka haitoweza
kuongeza muda watasitisha utoaji wa huduma kutokana na wamiliki wengi kuwa na
pikipiki zaidi ya moja na hivyo kushindwa
kumudu gharama za usajili.
Wameshauri ni vyema zoezi hilo
kuongezwa miezi sita zaidi ili kuwapa nafasi wamiliki kubadilisha vyombo vyao
na kuacha kuingia katika mgogoro na madereva
jambo ambalo linaweza kuwaathiri watumiaji wa kipato cha chini.
“Vipato vyetu kwa siku ni vidogo
tofauto na wamiliki wa magari na utakuta baadhi ya siku kunabeba abiria watu au
watano ambao hawakidhi mahitaji ya chombo wala ya familia zetu” alisema Bakari
Kimwaga
“Serikali inalazimka kuangalia
vipato vyetu tunavyopata kwani kuna baadhi ya watu wengine wanamiliki pikipiki
zaidi ya tatu na ukiangalia muda uliowekwa ni mdogo----tunaomba kuongezewa muda
zaidi” alisema
Akizungumza katika kongamano
hilo mmiliki wa bodaboda mbili, Rajab Shamte, alisema
kuweka muda maalumu wa mwisho wa kubadilisha namba hizo ni ukandamizaji na
kupendekeza pikipiki mpya ndizo ambazo zinatakiwa kuwa utaratibu huo.
Alisema kuna vyombo vingi ambavyo
baadhi yake vimekuwa chakavu na wamiliki
wake wanaweza kushindwa kumudu gharama za usajili na hivyo kuwawia vigumu.
Alisema ili kuwapa unafuu wamiliki wa pikipiki ni
vyema Mamlaka ya Mapato Tanzania kuongeza muda wa usajili vyenginevyo wanaweza kuingia mzozo na madereva.
Mwisho
No comments:
Post a Comment