Sunday, October 4, 2015

HASHIMU RUNGWE WA CHAUMMA AUNGURUMA UWANJA WA TANGAMANO, TANGA


Tangakumekuchablog

Tanga,MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Hshimu Rungwe, amesema endapo Watanzania watamchagua kuwa Rais  atahakikisha  anafufua viwanda na bandari zilizokufa.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni leo uwanja wa Tangamano, Rungwe, alisema Tanga ulikuwa mji wa viwanda na usafiri wa reli ambavyo vyote vimekufa jambo ambalo wananchi wake wamerudi katika umasikini na watu kuukimbia.

Alisema uwezo wa kuurejesha mji wa Tanga katika nafasi yake ya viwanda na usafirishaji wa shehena kwa kutumia bandari yuko nao hivyo kuwataka wananchi kumpa kura kwa wingi na kuweza kuongoza nchi.

“Mji wa Tanga ulikuwa unasifika kuongoza kwa viwanda na hakuna ubishi hapa kulikuwa hakuna umasikini-----wageni walikuwa wanamiminika na umasikini hapa haukuwepo” alisema Rungwe na kuongeza

“Musifanye kosa kuchagua kiongozi ambaye hana uchungu na wananchi----natambua hapa vyote toka mumekunywa chai na andazi moja au mawili asubuhi hamjala uwongo kweli” aliuliza

Akizungumzia bandari ya Tanga, Rugwe alisema imeshindwa kufanya kazi kutokana na viongozi kung’ang’ani bandari ya Dar es Salaam na kusababisha msongomano na foleni barabarani na kuwa usumbufu kwa wananchi.

Alisema atahakikisha bandari hiyo inafanya kazi kama ilivyo bandari ya Dar es Salaam  kwa meli kubwa kushusha shehena na kuwavutia wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi.

Alisema hakuna sababu ya wafanyabiashara wa Tanga kushusha mizigo yao bandari ya Dar es Salaam wakati Tanga ipo na kudai kuwa hapo kuna ukiritimba ambao akiwa Rais atauondosha.

“Bandari  yenu inakimbiwa na hata wafanyabiashara wa hapahapa munajua kwanini----ni ukiritimba ambao mimi naujua hivyo nipeni kura nyingi niwe kiongozi wenu muone Tanga itakavyopendeza” alisema Rungwe

Aliwataka vijana wazee na makundi yote ya walemavu kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura na kumchagua yeye kuwa Rais wao na kuondosha umasikini ambao kila siku umekuwa ukikua na kuwaumiza wananchi.
                                                     Mwisho

 Mgombea Urais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chaumma, Hashimu Rungwe akimtangaza mgombea Udiwani kata ya Mzizima  wa Chama hicho, Bakari Hamis wakati wa mkutano wake wa kujinadi kupitia nafasi hiyo ya Urais uwanja wa Tangamano








No comments:

Post a Comment