Sunday, October 11, 2015

MGOMBEA UDIWANI WA ACT-WAZALENDO KUMBE NAE YUMO



Tangakumekuchablog
Tanga,MGOMBEA Udiwani kata ya Mnyanjani kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Suleiman Khafidh, amesema endapo wananchi  watamchagua kuwa diwani atanunua helkopta kwa ajili ya wajawazito na wazee kuwapeleka hospitali.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni juzi uwanja wa mpira wa Mnyanjani, Khafidh alisema ili kukomesha wajawazito kujifungua njiani kutokana na mitikisiko ya ubovu wa  barabara  atawachukua kwa helkopta kutoka  nyumbani hadi hospitali.
Akitoa kali hiyo aliwafanya wananchi kumshangilia na kutakiwa kuitekeleza ahadi hiyo mapema ili kuweza kuvuna wanachama na kuwa na uhakika wa kuinyakua kata hiyo ya uwakilishi kupitia halmashauri.
“Ndugu zangu wananchi mimi ndie mgombea mdogo kuliko wagombea wote wa nafasi ya ubunge na udiwani hivyo damu yangu inachemka----akili za kijana ikiwaza na kudhamiria  ni kutekeleza tu” alisema Khafidh na kuongeza
“Nawaahidi mama zangu na wazee wangu wa kata hii endapo mutanichagua kuwa diwani wenu nitanunua helkopta kwa ajili yenu na kuwapeleka juu kwa juu hadi hospitali na kuondokana na adha ya ubovu wa barabara ambapo wakati mwengine wajawazito hujifungua barabarani” alisema
Akizungumzia fursa kwa vijana, mgombea huyo alisema atajenga shule maalumu ya lugha ya Kichina na Kiingereza ili kurahisisha mawasiliano katika nyanja za kibiashara na huduma za kijamii.
Alisema kundi kubwa la watu hasa vijana hawajui lugha za kigeni na badala yake wanashindwa kuwasiliana  na  watu wa mataifa mengine jambo ambalo limekuwa likiwapa nafasi wageni kuhodhi nafasi za ajira.
“Ndugu zangu niko na dhamira ya kweli kuifanya kata hii kuwa eneo la maendeleo ya kiuchumi na kijamii na kuwa mfano kwa kata nyengine----nitajenga chuo maalumu cha lugha ya kiingereza na kichina” alisema Khafidh
Alisema ili kuweza kuitekeleza dhamira yake hiyo amewataka wananchi kumpa kura nyingi kuwa Diwani wao na kusema kuwa atalipa fadhila hiyo kwa kutekeleza  ahadi zake kwa vitendo.
                                                           Mwisho

No comments:

Post a Comment