Wednesday, October 7, 2015

OMARI NUNDU AJITAPA, ADAI KUREJESHA VIBATI VYA NAMBA BARABARA ZOTE ZA NAMBA



Tangakumekuchablog
Tanga, MGOMBEA, Ubunge jimbo la Tanga mjini, Omari Nundu (CCM), amesema endapo atachaguliwa kwa mara nyengine tena atairejesha mitaa ya namba kama zamani na kuwataka wananchi kumchagua kwa kura nyingi.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni jana barabara ya 14 Ngamiani, Nundu alisema akichaguliwa atazirejesha barabara za namba kwa kubandika namba kila barabara kama ilivyokuwa zamani ili kuwarahisishia ufahamu wageni.
Alisema zamani mgeni akingia Tanga hakuhitaji kuuliza kwani kila barabara na mtaa kuna vibati ambavyo vinamuelekeza mtaa aliopo na kuwa rahisi kutambua aendako na kutokuwa na sababu ya kuuliza.
Alisema kwa sasa barabara hizo vibati vinavyoonyesha nambari za barabara zimeibiwa na kufanywa chuma chakavu jambo ambalo wageni linawapa shida kujua barabara aliyo na kulazimika kuuliza ambapo zamani zilikuwa zikiongoza.
“Nduguni nawaomba munichague tena kwa kura za kimbunga ili nikamilishe adhma yangu ya kuwaletea maendeleo nikiwa nanyi----miongoni mwa hayo ni kuzirejesha nambari za barabara kama ilivyokuwa zamani” alisema Nundu na kuongeza
“Zamani mgeni hakuwa na shida ya kukatisha mitaa kwani ilikuwa  inamuongoza kule aendako----- hivyo vimeibiwa na kufanywa chuma chakavu na niwaahidi kuwa nitalirejesha jiji katika hadhi yake kama ilivyokuwa” alisema
Akizungumzia kuhusu huduma za kijamii, Nundu alisema atahakikisha vijiji ambavyo havijafikiwa na huduma ya maji safi na salama pamoja na umeme vinafikiwa ili kuleta maendeleo.
Alisema kwa kushirikia na Serikali na wananchi ndani ya miaka mitano maji na umeme utakuwa umefika vijiji vyote na hivyo kuwataka wananchi kumchagua kwa kura nyingi.
“Nichagueni mimi nimalize ahadi zangu ambazo uchaguzi mkuu uliopita niliwaahidi na kuzitekeleza lakini badi kiduchu-----hili linawezekana kama mutanichagua tena” alisema Nundu
Aliwataka wananchi kata ya Ngamiani kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura na kurejea sehemu zao za kazi na kusubiri matokeo na kuwaasa kuacha kudanganywa na kuacha kutopiga kura.
                                     Mwisho
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment